
Katika
hati ya mashtaka iliyosomwa mahakamani hapo na wakili wa serikali
Mwandamizi Ashura Mzava mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Janeth Mtega imedai
kuwa mshtakiwa ametenda kosa hilo kati ya Januari mosi na Februari 26
mwaka 2020 huko katika eneo la Tabata, jijini Dar es Salaam.
Imedaiwa kuwa siku hiyo, mshtakiwa Daud alisambaza picha za ngono akitumia simu yake mkononi aina ya Tecno T301 kupitia akaunti ya Twitter yenye jina la James Michael @James Michae huku akijua kufanya hivyo ni kosa na kinyume cha sheria.
Hata hivyo mshtakiwa amekana kutenda kosa hilo na ameachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti aliyopewa likiwemo la kuwa na mdhamini mmoja wa kuaminika, ambapo yeye pamoja na mdhamini huyo walitaliwa kusaini bondi ya sh milioni 5.
Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamlika na kesi hiyo itatajwa Novemba 2 mwaka huu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...