Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
pamoja na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Bin Ally,
Balozi wa Morocco hapa nchini Abdelilah Benryane wakati alipotembelea
Msikiti Mkuu wa BAKWATA uliopo Kinondoni Muslim jijini Dar es Salaam
ambao umekamilika kujengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohamed VI wa Morocco
wakati akielekea Mburahati kwa ajili ya Mikutano ya Kampeni za Urais kwa
upande wa Chama cha Mapinduzi CCM leo tarehe 13 Oktoba 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
akimsikiliza Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Bin Ally
wakati alipotembelea Msikiti huo Mkuu wa Bakwata Kinondoni Muslim jijini
Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
akizungumza jambo wakati alipotembelea Msikiti Mkuu wa BAKWATA uliopo
Kinondoni Muslim jijini Dar es Salaam ambao umekamilika kujengwa kwa
ufadhili wa Mfalme Mohamed VI wa Morocco baada ya Mhe. Rais Magufuli
kumuomba Mfalme wa Morocco kuwajengea Waislamu Msikiti alipofanya ziara
hapa nchini tarehe 24 Oktoba, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mufti Mkuu wa
Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Bin Ally, Balozi wa Morocco hapa nchini
Abdelilah Benryane wakwanza kushoto, pamoja na viongozi mbalimbali wa
Bakwata mara baada ya kutembelea Msikiti Mkuu wa Bakwata uliokamilika
kujengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohamed VI wa Morocco.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
akiombewa Dua iliyokuwa ikiongozwa Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh
Aboubakar Zubeir Bin Ally mara baada ya kutembelea Msikiti Mkuu wa
Bakwata uliokamilika kujengwa kwa ufadhili wa Mfalme Mohamed VI wa
Morocco.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
akimsikiliza Balozi wa Morocco hapa nchini Abdelilah Benryane wakati
alipokuwa akielezea ujenzi huo wa Msikiti mpya uliokamilika kujengwa
katika Makao makuu ya Bakwata Kinondoni jijini Dar es Salaam.
PICHA NA IKULU
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...