Na Mwandishi wetu, Kiteto

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU kwa kushirikiana na jeshi la polisi wamemfikisha mahakamani mkazi wa Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, Moita Tapeno Paparai kwa kutumia jina la Mkuu wa Wilaya ya Kiteto kanali Patrick Songea na kujipatia shilingi laki tano.

Mwendesha mashtaka wa polisi D/C Ramadhan akisoma hati ya mashtaka mbele ya hakimu mkazi wa wilaya hiyo Mossy Sasi, amesema Moita amefanya kosa hilo kinyume cha kifungu cha 302 cha kanuni ya adhabu.

D/C Ramadhan amesema katika kesi hiyo namba CC 22/2020 pamoja na shtaka hilo pia Moita ameshtakiwa kwa kosa lingine la pili.

Amesema mshtakiwa huyo alijifanya Ofisa ustawi wa jamii kinyume cha kifungu cha 100 kanuni ya adhabu.

Hata hivyo, Moita alikana mashtaka hayo pindi alipoulizwa mahakamani hapo kama ni kweli ametenda kosa hilo.

Mshtakiwa huyo alipelekwa mahabusu kwenye gereza la wilaya ya Kiteto, baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana hadi Octoba 21 kesi hiyo itakapotajwa tena.

Mkuu wa TAKUKURU Mkoani Manyara, Holle Joseph Makungu ametoa rai kwa wananchi kuiga mfano wa mwananchi aliyetoa taarifa za Paparai kwenye ofisi ya TAKUKURU kwa kutokubali kutoa fedha kwa kisingizio cha kutumwa na viongozi wa Serikali.

Makungu amesema wananchi wanapaswa kutoa taarifa TAKUKURU au kituo cha polisi katika eneo la karibu ili hatua ziweze kuchukuliwa kama ilivyofanyika kwa Moita.

Mkazi wa Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, Moita Tapeno Paparai amefikishwa mahakamani kwa kosa la kutumia vibaya jina la Mkuu wa Wilaya ya Kiteto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...