Na Amiri Kilagalila,Njombe
Waziri wa kilimo nchini Tanzania Japhet Hasunga ameongoza zoezi la uzinduzi mpango jumuifu yenye lengo la kuwaelimisha wataalamu na wananchi jinsi ya kuzalisha,kuhifadhi na kutumia mazao mbali mbali ili kuboresha lishe na kipato katika ngazi ya kaya na kitaifa.
Serikali imezindua miongozo ya kanuni na tekinolojia bora ya uzalishaji na usimamizi wa mazao ya Pili pili hoho,mboga za majani,Bamia,Nyanya,Karoti,
Uzinduzi huo umefanyika mkoani Njombe kabla ya kuhitimisha kilele cha siku ya chakula Duniani ambayo kitaifa imefanyika mkoani Njombe katika halmashauri ya mji wa Njombe.
Lakini vile vile serikali imezindua muogozo wa kufundisha uzalishaji na usimamizi wa zao la mpunga kwa ajili ya matumizi mbali mbali.
Aidha waziri Hasunga ametumia fursa hiyo kuwaomba wadau kutumia miongozo hiyo kuwaelimisha wananchi ili kuhakikisha wanakabiliana na changamoto kwenye kilimo


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...