**************************************

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Aboubakar Kunenge leo ameshiriki hafla ya Mwaka Mpya wa Kihindu ambapo ametoa wito kwa Wahindi na wananchi kwa ujumla kuendelea kumuombea Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Katika Muhula wa pili wa uongozi ili aweze kutimiza yote aliyoahidi.

Aidha RC Kunenge ametoa Rai kwa wananchi wa Mkoa huo kulipa Kodi ili kuiwezesha Serikali kutoa huduma Bora kwa Wananchi.

Katika mahadhimisho hayo yaliyofanyika Jijini Dar es salaam, RC Kunenge amewataka Wahindi kuchangamkia fursa zote zinazopatikana nchini na kuhakikisha wanazingatia sheria.

Pamoja na hayo RC Kunenge amesema Serikali imejipanga kuhakikisha inasimamia suala la Amani na Utulivu Jijini humo ili kila mmoja aweze kufanya Shughuli zake kwa usalama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...