Jonas Kamaleki, Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameahidi kuboresha mazingira ya kazi pamoja na maslahi ya watumishi wetu wote ili yaendane na hali halisi ya maisha ya Watanzania.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo bungeni jijini Dodoma wakati akizindua Bunge la 12 ambalo ameahidi kushirikiana nalo kwa karibu.

“Tutaendelea kuboresha mazingira ya kazi pamoja na maslahi ya watumishi wetu wote ili yaendane na hali halisi ya maisha ya Watanzania, kwa hiyo, watumishi wasiwe na wasiwasi”, alisema Rais Magufuli.

Kuhusu utawala bora katika miaka mitano ijayo, Rais Magufuli ameahidi kuendelea kusimamia nidhamu kwenye utumishi wa umma pamoja na kuzidisha mapambano dhidi ya rushwa, wizi, ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma.

Aliongeza kuwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Serikali iliwachukulia hatua za kinidhamu watumishi 32,555 na kuiwezesha Tanzania kushika nafasi ya kwanza kati ya nchi 35 za Afrika kwa kupambana na rushwa, kwa mujibu wa Transparency International; na pia kushika nafasi ya 28 kati ya nchi 136 duniani kwa matumizi mazuri ya fedha za umma kwa mujibu wa Utafiti Jukwaa la Dunia (World Economic Forum) wa mwaka 2019.

Bunge la 12 lililozinduliwa leo Novemba 13 na Rais Magufuli, limeahirishwa  hadi Februari 2, 2021 saa tatu asubuhi.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli

 

 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...