Waziri
wa Maji Jumaa Aweso amewataka Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira
Dar es Salaam (DAWASA) kuendeleza jitihada ili wananchi wapate huduma
ya maji safi na salama.
Hayo
ameyasema wakati wa ziara ya kutembelea mradi wa maji wa Kisarawe-
Pugu-Gongo la Mboto utakaohudumia wananchi wa Pugu hadi Tabata.
Katika
ziara hiyo, Waziri Aweso alitembelea tanki la kuhifadhia maji na
kushuhudia maji yakianza kuingia kwenye pamoja na kuzindua maji eneo la
Kifuru.
Akizungumza
na waandishi wa habari Leo Jijini Dar es Salaam, Aweso amesema Dawasa
wanafanya kazi nzuri sana chini ya Afisa Mtendaji Mkuu Mhandisi Cyprian
Luhemeja kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuhakikisha wananchi wa mkoa wa
Dar es Salaam na Pwani wanapata maji safi na salama.
Amesema,
" DAWASA wametekeleza agizo la Rais wetu kwa kufikisha huduma ya Maji
safi kwa wakazi wa Pugu ,Gongo la mboto, Majohe, Chanika,Ukonga na
Segerea kabla ya Disemba 25 Mwaka huu, limetekelezwa,"
Aweso
amesema, pia ameona maendeleo mazuri katika mradi huo naada ya
kutembelea Mradi wa Ujenzi wa Tank kubwa la Maji linalopokea maji kutoka
Kisarawe kwenda Pugu lenye uwezo wa kupokea na kusambaza Lita milioni
2.8 kwa siku lililojengwa kwa thamani ya shilingi bilioni 6.9 lililoanza
kupokea maji na kusambaza kwa wananchi.
Mradi
huo utahudumia wakazi wa Jimbo la Ukonga ikiwemo Pugu, Majohe, Gongo la
mboto, Bangulo, Airwing, Kigogo, Chanika, Kinyamwezi, Banana, Segerea
na Kifuru.
Aweso
ameonyesha kufurahishwa na utekelezaji wa agizo hilo ndani ya muda
mfupi na kuwataka DAWASA kuwekeza nguvu zaidi katika kuwaunganishia
wananchi huduma hiyo ili kila mwananchi awe na huduma.
"Mradi
huu tumeutekeleza Wizara kupitia DAWASA na ni faraja kwetu kuwa
umekamilika ndani ya wakati na unaenda kuondoa shida yote ya Maji kwa
maeneo yaliyopitiwa na mabomba hayo kuanzia Pugu hadi Kinyerezi"amesema
Aweso
Kwa
upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge ametoa wito
kwa wananchi kulipa bili za Maji ili kuiwezesha DAWASA kuendelea
kupanua huduma kwani miradi mingi inayofanywa na Mamlaka hiyo inatumia
fedha zake za ndani zitokananazo na makusanyo ya ankara za huduma ya
Maji.
Aidha
Kunenge amesema Serikali itawachukulia hatua za kisheria wezi wa maji
na wanaoharibu miundombinu ya Maji huku akiwaelekeza DAWASA kudhibiti
tatizo la upotevu wa Maji.
Mradi
wa Maji Kisarawe-Pugu - Gongo la mboto umetekelezwa na DAWASA baada ya
kukamilika kwa mradi mkubwa wa maji Kibamba- Kisarawe ulioleta uhitaji
kwa wananchi wa maeneo hayo.
Jumla ya shilingi Bilioni 6.9 zimetumika hadi kukamilisha kwa mradi huo utakaonufaisha wakazi takribani 450,000.
Waziri
wa Maji Jumaa Aweso akifunga mita ya maji wakati akizindua huduma ya
maji kwa wananchi wa Kifuru kupitia mradi wa maji wa Pugu - Gongo la
Mboto ulioanza kufanya kazi baada ya kukamilika kwa ujenzi wa tanki la
kuhifadhia maji Pugu. Waziri Aweso aliambatana na Mkuu wa Mkoa Dar es
Salaam Abubakar Kunenge, Mbunge wa Segerea Bonna Kamoli, Makamu
Mwenyekiti wa Bodi na viongozi wengine
Waziri
wa Maji Jumaa Aweso akipata maelezo ya mradi wa maji Pugu-Gongo la
Mboto kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakati wa kutembelea mradi huo ulioanza kutoa huduma kwa wananchi wa
Gongo la Mboto hadi Kifuru, Katika ziara hiyo aliambatana na Mkuu wa
Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge, Mbunge wa Segerea Bonna Kamoli
pamoja na viongozi wengine wa serikali na DAWASA.
Waziri
wa Maji Jumaa Aweso na Afisa Mtendaji Mkuu DAWASA Mhandisi Cyprian
Luhemeja wakipandisha juu ya tanki la maji kwa ajili ya kulikagua na
kuona namba maji yalivyoanza kuingia.
Waziri
wa Maji Jumaa Aweso akiangalia namna maji yanavyoingia katika tanki la
kuhifadhia maji la Pugu likipokea kutoka tanki la Kisarawe kwa ajili ya
kuwahudumia wananchi wa Pugu-Gongo la Mboto na kupata maelezo kutoka
kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja wakati wa
kutembelea mradi huo ulioanza kutoa huduma kwa wananchi wa Gongo la
Mboto hadi Kifuru, Katika ziara hiyo aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dar
es Salaam Abubakar Kunenge, Mbunge wa Segerea Bonna Kamoli pamoja na
viongozi wengine wa serikali na DAWASA.
Waziri wa Maji Jumaa Aweso akimtwisha mama ndol ya maji kichwani baada ya kuzindua rasmi huduma ya maji Segerea mtaa wa Kifuru.
Waziri wa Maji Jumaa Aweso akipata maelezo ya mradi wa maji Pugu-Gongo
la Mboto kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian
Luhemeja wakati wa kutembelea mradi huo ulioanza kutoa huduma kwa
wananchi wa Gongo la Mboto hadi Kifuru, Katika ziara hiyo aliambatana
na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge, Mbunge wa Segerea
Bonna Kamoli pamoja na viongozi wengine wa serikali na DAWASA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...