MFANYABIASHARA anayeishi Kinondoni Bwawani jijini Dar es Salaam,  Benedict Kimbusu, amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shtaka kusambaza maudhui mtandaoni bila ya kuwa na kibali.

Katika hati ya mashtaka iliyosomwa mahakamani hapo na wakili wa serikali Adolph Ulaya, mbele ya Hakimu Mfawidhi Yusto Ruboroga imedai kuwa mshtakiwa ametenda hilo, kati ya Februari 27, 2014 na Desemba 7 mwaka huu ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Imedaiwa, siku hiuo, mshtakiwa alisambaza maudhui kupitia Chanel ya YouTube iitwayo Pioh the 9os Lyrics bila ya kuwa na kibali kutoka mamlaka ya mawasiliano TCRA.

Hata hivyo mshtakiwa amekana kutenda kosa hilo na yuko nje kwa dhamana ya kufanikiwa kutimiza masharti ambayo yaliyomtaka kuwa na wadhamini watakaosaini bondi Bondi ya sh. Milioni tatu. Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na kesi hiyo imeahirishwa Desemba 30, mwaka huu.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...