Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais - Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo amezitaka Taasisi za Fedha nchini kuhakikisha zinasaidia na kuwasukuma Wafanyabiashara wadogo kwa kuwapa mitaji ili kufikia malengo ya Uwekezaji nchini.

Prof. Kitila ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika Taasisi mbalimbali za Fedha za TIB, Shirika la Maendeleo nchini (NDC) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB).

Prof. Kitila amezitaka Taasisi hizo kuhamasisha Wafanyabiashara hao ambao wanaojihusisha na uuzaji na uchuuzi ambao hawazalishi mazao.

Pia Prof. Kitila amezitaka Taasisi hizo kuwasukuma Wafanyabiashara wadogo ili wafanye biashara hizo na baadae zitambulike ili kufikia malengo ya biashara za Viwanda vidogo vya utengenezaji na uzalishaji ili na wao wazalishe Ajira kwa wengine.

Kwa upande wake Mkrugenzi Mtendaji wa Benki ya TIB, Charles Singili amehakikisha suala la kujitangaza zaidi kwa Wawekezaji baada ya Serikali na Waziri mwenye dhamana ya Uwekezaji Prof, Kitila kuhimiza suala hilo la kujitangaza kwa Taasisi hiyo ili kuvutia zaidi Uwekezaji na kukuza uchumi wa nchi maendeleo ya Taifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo, Japhet Justine wamehakikisha kwa Waziri Prof Kitila na Serikali kutoa mitaji kwa Wafanyabiashara na kuwasaidia Watanzania katika Bishara zao ili kukuza Uwekezaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...