Mwenyekiti wa Bodi Ya Wakurugenzi wa TAWA Meja Jenerali Mstaafu Hamis R. Semfuko akinunua Nyamapori kihalali kumuunga mkono Mfanyabiashara wa Bucha hiyo ya Nyamapori  na baadae kukabidhiwa risiti za mashine ya EFD.

 

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TAWA Meja Jenerali Mstaafu Hamis R. Semfuko Leo tarehe 20/12/2020 Jijini Dodoma amezindua bucha ya kwanza ya nyamapori nchini kufuatia agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli alilolitoa mapema mwaka huu.

Hafla hizo za Uzinduzi zilifanyika maeneo ya chang'ombe Mtaa wa Stendi ya Zamani Makao Makuu ya Nchi Dodoma, ambapo Mwenyekiti huyo wa Bodi aliambatana na Kaimu Kamishna wa Uhifadhi Bw. Mabula Misungwi pamoja na wajumbe wa Bodi hiyo ya TAWA.

Aidha, bucha hii imekuwa ya kwanza kati ya bucha 46 zilizopata usajili baada ya Kamati ya Kumshauri Kamishna kuhusu bucha za kuuza nyamapori kuridhia kufuatia kanuni ya  bucha ya mwaka 2020  ambayo iliundwa baada ya Tamko la Mh.Rais Dkt.John Pombe Joseph Magufuli la Mwezi  Machi mwaka huu kutaka kuanzishwa bucha za nyamapori Tanzania.

Wananchi wa Viunga vya jiji la Dodoma leo walifurika maeneo ya chang'ombe kushuhudia zoezi hilo la Uzinduzi na kufurahia fursa ya kupata kitoweo adimu cha Nyamapori, ambapo Mara baada ya zoezi la Uzinduzi wananchi hao walijaa katika bucha hiyo inayomilikiwa na Mfanyabiashara aitwaye Bw.Samson Joel  Kitangengi na kujinunulia kitoweo hicho.

TAWA imetekeleza kikamilifu agizo la Rais wetu na hivyo ni imebaki zamu ya wananchi wa Tanzania kufurahia fursa hadhimu ya  rasilimali za wanyamapori wetu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...