Na Mwandishi wetu, Manyara

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa chama cha ushirika cha Rift Valley Cooperative Union (RIVACU) Lohay Langay anashikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU kwa kutoa ajira bila idhini ya bodi ya wakurugenzi wa chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Babati, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara, Holle Joseph Makungu amesema Langay anatuhumiwa kufanya kosa hilo Novemba mosi mwaka 2017 akiwa Mwenyekiti wa RIVACU.

Makungu amesema Langay akiwa Mwenyekiti wa RIVACU alitumia vibaya nafasi yake kwa kuingia mkataba wa ajira ya uhasibu kwa Paul Makoye bila idhini ya bodi ya wakurugenzi wa chama hicho cha ushirika.

"Katika uchunguzi wetu tumebaini kuwa katika mkataba huo Makoye aliingia mkataba bila idhini ya bodi ya wakurugenzi wa chama hicho cha ushirika na kujipatia ujira usio wa haki wa shilingi milioni 2.6," amesema Makungu.

Amesema kitendo cha kuajiri bila kibali ni kosa la matumizi mabaya ya ofisi kinyume na kifungu cha 31 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007.

"Langay anatarajiwa kufikishwa kwenye mahakama ya hakimu mkazi wa mkoa wa Manyara na kusomewa shtaka hilo na mwendesha mashtaka wa TAKUKURU Wakili Martin Makani," amesema Makungu.

 Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara Holle Joseph Makungu akizungumza na waandishi wa habari Mjini Babati.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...