Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cypriani Luhemeja alisema kazi ya ulazaji wa miundombinu ya maji katika maeneo hayo imeanza na kwamba wananchi katika wilaya ya Mwanga na Same wataanza kupata huduma ya maji ifikapo Novemba 30 mwaka huu.
Waziri wa Maji Jumaa Aweso akiwa ameongozana na viongozi mbalimbali wakiwemo wataalamu kutoka taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maji wakati akitembelea maeneo mbalimbali kujionea sehemu ya mradi wa maji wa Same -Mwanga -Korogwe uliokua umesimama
Waziri wa Maji Jumaa Aweso akitizama moja ya chujio la maji katika mradi mkubwa wa Maji wa Same- Mwanga- Korogwe alipotembelea pamoja na wataalamu kutoka katika wizara hiyo.
Waziri wa maji Jumaa Aweso akiwa katika eneo la kupolelea maji kutizama namna ambavyo wataalamu wa ndani wanaweza kuendeleza kazi hiyo ambayo kwa sasa imekabidhiwa rasmi kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)
Waziri wa Maji Jumaa Aweso akizungumza wakati wa hafla fupi ya utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Same -Mwanga -Korogwe ,mradi ambao sasa umekabidhiwa kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) .
Baadhi ya Watendaji kutoka Wizara ya Maji wakiwa katika hafla fupi ya utekelezaji wa mradi huo ,hafla iliyofanyika katika ofisi za Mamlaka ya Maji ya Same Mwanga .
Katibu Mkuu Wizara ya Maji ,Mhandisi Anthony Sanga akizungumza katka hafla hiyo ambapo aliwanyooshea kidole wahandisi watakao suasua katika utekelezaji wa miradi ya maji kote nchini ,
Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa ,Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza katika hafla hiyo ambapo amewatoa hofu wakazi wa wilaya za Mwanga na Same kuhusu huduma ya Maji na kwamba ifikapo Novemba 30 mwaka huu wateja 100 kwa wilaya ya Mwanga na wateja 100 kwa wilaya ya Same watakua wanatumia maji safi na salama.
Baadhi ya Wananchi waliohudhuria hafla hiyo wakifuatilia hotuba mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na viongozi .
Waziri wa Maji Jumaa Aweso akikata utepe kuashiria kuanza rasmi kwa utekelezaji wa mradi wa MAji wa Same -Mwanga -Korogwe muda mfupi baada ya kukabidhiwa kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) .
Waziri wa Maji Jumaa Aweso akiunganisha moja ya mabomba yaliyoanza kusambazwa katika mji wa Mwanga mara baada ya mradi huo sasa kikabidhiwa Dawasa.
Wakuu wa wilaya za Mwanga na Same Thomas Apson na Rosemery Senyamule wakishirikiana na wananchi wengine kufukia mitaro ambayo tayari bomba za maji zimewekwa.
Baadhi ya Wananchi wakishiriki katika kazi ya kujitolea kwa kufukia mtaro kulikolazwa Bomba mara baada ya mrad huo kukabidhiwa Dawasa.
Sehemu ya Mradi wa Maji wa Same Mwanga Korogwe unavyoonekana kwa juu ,mradi ambao sasa umekabidhiwa Dawasa.
Na Dixon
Busagaga-Mwanga
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...