Baadhi ya maeneo ya kati ya taifa la Msumbiji yamekumbwa na mafuriko baada ya kimbunga Eloise kupiga eneo lililo karibu na mji wa Beira na upepo wenye kasi ya kilomita 160 kwa saa .
Beira ilipokea milimita 250 za mvua katika kipindi cha saa 24 , kulingana na Taasisi ya kitaifa ya hali ya hewa nchuni humo INAM.
Baadhi ya maafisa na mashirika ya misaada yanachunguza kiwango cha uharibifu huo ili kuweza kuwasaidia walioathirika, na kujaribu kurudisha umeme na mawasiliano ambayo yalikatwa katika baadhi ya maeneo. Watu wameuawa kulingana na maafisa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...