ALIYEKUWA kocha wa Simba SC, Mbelgiji Sven Ludwig Vandenbroeck amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na ASFAR Rabat ya Morocco.

Vandenbroeck amejiunga na timu hiyo Rabat siku moja mbili baada ya kuondoka Simba SC akitoka kuiwezesha kufuzu Hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Jumatano ikiitoa FC Platinum kwa jumla ya mabao 4-1.

Katika kipindi cha mwaka mmoja na zaidi ya kuwa na Simba, Vandenbroeck ameiwezesha timu hiyo kushinda mataji matatu, Ngao ya Jamii, Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC.)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...