Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar  Maalim Seif Sharif Hamad ameyasema hayo katika Mkutano wa ZANZIBAR PEACE CONFERENCE ambao umeandaliwa na taasisi ya FRIENDS OF ZANZIBAR wakishirikiana na Ofisi ya Mufti Zanzibar leo tarehe 16/01/2021.

Mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Beach Resort iliyopo Mazizini Mkoa wa Mjini Magharib Unguja, umewakutanisha Wawakilishi wa kibalozi na taasisi nyengine mbalimbali ambao ni wajumbe wa taasisi ya Friend of Zanzibar.

Wawakilishi hao wametoa salamu zao sambamba na kusema kwamba wao wapo pamoja na Taifa la Zanzibar na wanawapongeza sana Viongozi kwa kushirikiana na kuleta amani katika Nchi hii.

Pamoja na hayo wageni hao wamesema hata wao wanaamini kwamba ushirikiano uliopo Zanzibar kwa sasa ni ujumbe mzuri kwa Mataifa mengine mengi ya bara la Africa.

Nae Maalim Seif katika kutoa salamu zake kwa Wajumbe hao alisema;
 "Katika Nchi mbalimbali migogoro huwa haiachi kutokea, lakini inapotokea kuna njia mbili hutumika, ya kwanza nikupigana hadi kuumizana ndio mwisho viongozi hukaa kwenye meza kutafuta suluhu, na nyengine ni kuepuka kugombana na mukakaa kwenye meza kuyatatua, na sisi Zanzibar tuliamua kukaa kwenye meza moja kuyajadili bila ya kuumizana na ndio njia nzuri zaid".

Maalim alitoa nasaha zake kwa Mgeni rasmi wa Mutano huo Rais Mwinyi kwa kumwambia;
"Mh. Rais maridhiano nikama mtoto ambae ni mwema, hivyo tunahitaji kumlea vyema ili vizazi vyetu vije kuirithi amani hii sambamba na kuiacha Zanzibar kuwa ni Nchi ya amani na iliyo salama".

Mwisho Maalim Seif  aliwashukuru sana taasisi ya Friend wa Zanzibar kwakusema;

 "Anaekufaa kwa dhiki ndio rafiki, na taasisi hii iliyokusanya wajumbe wa Mataifa mbalimbali nawashukuru sana kuwa pamoja nasi na kuendelea kuwa marafiki zetu hata wakati wa matatizo".






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...