Naibu waziri ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe David Silinde (Mb) ameipongeza wilaya ya Arumeru pamoja na Halmashauri zake mbili za Meru Dc na Arusha Dc kwa kazi ya ujenzi wa madarasa pamoja na usimamizi madhubuti wa fedha za Umma za miradi ya EP4R
Mhe Silinde ambae amefanya ziara leo Tarehe 14/01/2021 katika wilaya ya Arumeru ameonyeshwa kuridhishwa kwa kiwango kikubwa cha namna Halmashauri za Meru Dc na Arusha Dc zilivyoweza kutekeleza kwa vitendo maagizo ya Mhe Waziri Mkuu Kasim Majaliwa Majaliwa ya ujenzi wa madarasa ambayo kwa Wilaya ya Arumeru madarasa yote yanayojengwa ni ya kisasa kwa gharama nafuu
Katika hatua ingine Mhe Silinde ameonyesha kufurahishwa na maamuzi ya ujenzi wa madarasa kwa mtindo wa magorofa unaofanywa na Halmashauri ya Arusha Na Meru hatua inayosaidia kuondokana na changamoto ya uhaba wa Ardhi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...