Hayo yamesemwa mjini Morogoro jana na Katibu wa Shirikisho la Vyama vya tiba asili nchini,
Othaman Shem, wakati wa maonesho ya mimea dawa kwa wadau wa tiba asili
yaliyoandaliwa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo.
Akizungumza na
waandishi wa habari kwenye maonesho
hayo, Shem alisema kuwa gharama kubwa za usajili wa dawa za asili imekuwa ni
kikwazo kwa wataalamu wa tiba asili kuweza kuingiza dawa hizo kwenye soko la
ndani na nje ya nchi.
“ Tiba asili zina umuhimu mkubwa na zinafanya kazi nzuri ya kutibu
sawasawa na hata kuzidi tiba za kisasa. Kikwazo kikubwa kwa tiba asili kusambaa
kwa wingi nchini ni gharama kubwa za
usajiri wa dawa hizo ili ziweze kukubalika kwa matumizi na kuingia
sokoni.” Alisema Shem.
Shem alisema kuwa
kusajili aina moja ya dawa ya asili ili
iweze kukubalika kisheria ni Shilingi 1.5 Milioni, kiasi ambacho amekitaja kuwa
ni kikubwa mno kwa wataalamu wa tiba asili kuweza kumudu.
“ Ni vema serikali ikatazama upya sheria, vigezo na gharama za usajili wa dawa
za asali. Tunao wataalamu wengi wa tiba asili ambao dawa zao zina uwezo mkubwa
wa kutibu magonjwa mbali mbali lakini wanakwazwa na gharama kubwa , sheria na
mlolongo mrefu wa usajili.” Alisema.
Shem alitolea mfano
wa sheria namba 23 ya tiba asili ya mwaka 2002, iliyofanyiwa marekebisho mwaka
2017 kuwa sio rafiki kwa wataalamu wa tiba asili kwa kuwa pamoja na vipengele
vingine ambavyo sio rafiki ina kipengele kinachozuia kutangaza tiba asili jambo
ambalo amelilalmikia.
Katika hatua nyingine
Shem ameishauri serikali kufanyia mrekebisho muundo wa baraza la tiba asili kwa kuwaondoa wote ambao sio wataalamu wa tiba hizo.
“ Baraza la tiba asili linaundwa na Madaktari wa tiba za
kisasa, hii sio sahihi kabisa, tunatoa wito kwa serikali kufanya marekebisho wa
muundo wa baraza hilo ili liundwe na wataalamu wa tiba asili..” Alisema Shem.
Naye Kaimu Naibu
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine
cha Kilimo, anayeshughulikia taaluma, Profesa Samwel Kabote, akizungumza kwenye
maonesho hayo aliwashauri wataalamu wa tiba asili na wadau wote nchini
kuanzisha vitalu na kupanda mimea tiba ili kuepuka na uharibifu wa mazingira
kwa kuvuna mimea hiyo kwenye misitu ya
asili au misitu ya hifadhi.
“ Kadri miaka
inavyokwenda miti ya mimea tiba inakwisha, hivyo ni vyema wadau wa dawa za
asili wakaanza kufikiria kuanzaisha vitalu vya mimea tiba kwa ajili ya kuifanya
mimea hiyo kuwa endelevu.
Profesa Kabote alisema
kuwa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo ina kitengo maalum kwa ajili ya utafiti
wa mimea tiba na kinatoa ushauri kwa wadau wanaotaka kuanzisha vitalu vya mimea
tiba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...