Na Mwandishi wetu, Simanjiro
TAASISI
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU imewafikisha Mahakamani
waliokuwa viongozi sita akiwemo Mwenyekiti wa Kijiji cha Kilombero
Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, kwa shataka la kuuza ekari 810 bila
idhini ya mkutano Mkuu wa Kijiji.
Hata
hivyo, washtakiwa wawili hawakuwepo Mahakamani hapo hivyo wanaendelea
kutafutwa ili waunganishwe na wenzao kwenye kesi hiyo.
Washtakiwa
hao wanne wamefikishwa kwenye mahakama ya hakimu mfawidhi wa mahakama
ya Wilaya ya Simanjiro, Charles Uiso na kusomewa mashtaka hayo na
mawakili wa TAKUKURU, Adam Kilongozi na Martin Makani, leo January 20.
Washtakiwa
wa kesi hiyo namba 12/2021 ni ofisa mtendaji wa kijiji hicho, Emmanuel
Komba, aliyekuwa Mwenyekiti wa kijiji hicho Jamhuri Munna na waliokuwa
wjumbe wanne wa serikali ya kijiji hicho.
Wajumbe hao ni Habibu Dimbui, Robert Matua, Sara Isack na Hatibu Rajabu.
Waendesha
mashtaka hao, wamedai kwamba mshtakiwa Komba aliuza ekari 400 yaa ARDHI
bila idhini ya mkutano Mkuu wa kijiji na kuwezeshwa aliyekuwa
Mwenyekiti wa Kijiji hicho Munna kujipatia faida isiyomstahili ya
shilingi milioni 114.5.
Wajumbe
hao wanne wanatuhumiwa kutumia madaraka yao vibaya kwa kuidhinisha
mauzo ya ekari 400 kinyume cha kifungu cha 31 cha sheria ya kuzuia na
kupambana na rushwa namba 11/2007.
Hata
hivyo, washtakiwa hao wamekana mashataka hayo mahakamani hapo na
wamepelekwa mahabusu mara baada ya kushindwa kupata dhamana na kesi hiyo
imeahirishwa hadi itakapotajwa tena Januari 21 mwaka huu mahakamani
hapo.
Washtakiwa wawili Komba na Dimbui ambao hawakuwepo mahakamani hapo wanaendelea kutafutwa ili kuunganishwa kwenye kesi hiyo.
Mkuu
wa TAKUKURU mkoani Manyara, Holle Joseph Makungu amedai kuwa uchunguzi
wa TAKUKURU umeonyesha Wilaya za Simanjiro na Kiteto na Kiteto, kumezuka
mtindo wa viongozi wa vijiji wakiwemo wenyeviti, watendaji na wajumbe
wa kamati ya ardhi kujipa mamlaka ya kuuza au kusimamia uuzaji ardhi ya
kijiji bila idhini ya mkutano mkuu wa kijiji.
Ametoa
rai kuwa katika uuzaji wa ardhi, wenyeviti wa vijiji, wajumbe wa kamati
za ardhi wazingatie sheria ya ardhi ya vijiji CPA 114 ambapo kijiji
kupitia mkutano mkuu wa kijiji umepewa mamlaka ya kuuza ekari 50 na siyo
vinginevyo.
Makungu
amesema wanaonunua ardhi hiyo kupitia uongozi wa kijiji bila kupitia
mkutano mkuu wa kijiji wafahamu kuwa wanalaghaiwa na mikataba ya uuzaji
huo ni batili.
"Kila
tunapowabaini wafahamu kuwa watapoteza fedha zao kutokana na manunuzi
hayo batili mbele ya sheria ya ardhi hivyo itarejeshwa kwenye umiliki wa
vijijin husika," amesema Makungu.
Mkuu wa TAKUKURU Mkoani Manyara Holle Joseph Makungu akizungumza na waandishi wa habari Mjini Babati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...