Na  Linda Shebby  Kibaha 

MENEJA wa Mamlaka ya Maji na Usafi   wa Mazingira (DAWASA ) Mkoa wa Kibaha Alfa  Amos  Ambokile  amesema kuwa  mradi wa maji  katika eneo la Pangani uko  kwenye hatua za mwisho huku akisisitiza kuwa utekelezwaji wakw umepangwa kufanyika katika kipindi cha mwaka mpa wa fedha utakao anza baadaye mwaka huu.

Meneja huyo alisema  hayo  kufuatia kuulizwa na wakaazi wa  eneo la Pangani ambao wamekua  wakikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji kwa muda mrefu sasa.

Alisema  eneo  la Disunyala nalo tayari michoro yake imekamilika katika mradi  wa kimkakati hivyo nao litashughulikiwa   katika mwaka wa fedha wa utekelezaji baadaye mwaka huu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika ofisi zao  zilizopo Wilayani Kibaha  Ambokile amesema  kuwa
"kwa maelezo mafupi naweza kusema kuwa hadi sasa  tayari miradi ambayo tayari imekamilika ni pamoja na Mradi wa maji Soga ambao umekamilika kwa asilimia 100 (100%)ambapo  wananchi tayari wameshaanza kupata huduma ya maji."

Aidha alitaja maeneo mengine ambayo ambayo kazi  zinaendelea ni  pamoja na Mbwawa ambapo  mradi  umekamilika kwa asilimia 80 (80%),  alisema kuwa katika eneo hili  zimebaki  maeneo  machache  huku akisisitiza kwamba  mafundi wako katika eneo husika wakiendelea na kazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...