KAMPUNI ya Mohamed Enterprises imetoa msaada wa vyakula na sabuni vilivyogharimu zaidi ya shilingi milioni 1.8 kwa vituo vitatu vya kulelea watoto yatima mjini Songea mkoani Ruvuma.

Mwakilishi wa Kampuni hiyo Angel Samasuba akizungumza  mara baada ya kumaliza zoezi la ugawaji wa msaada huo,amevitaja vituo vya kulelea yatima vilivyopata msaada huo kuwa ni Kituo cha SWACCO kilichopo Kata ya Mwengemshindo, St.Antony cha Mfaranyaki na Kituo cha Mchungaji Mwema kilichopo Mjimwema.

Samasuba amesema Kampuni ya Mohamed Enterprises katika vituo vyote vitatu imetoa jumla ya lita 120 za mafuta ya kula zilizogharimu shilingi  516,000 na mifuko ya unga wa sembe kilo 300 iliyogharimu shilingi 234,000.

Misaada mingine iliyotolewa ni sabuni za miche katoni 12 zenye thamani ya shilingi 120,000, juisi katoni 30 zenye thamani ya shilingi 195,000 na mbuzi sita wenye thamani ya shilingi 600,000.

“Sisi kama Kampuni ya Mohamed Enterprises tumekuwa na kawaida ya kutoa misaada kwa makundi maalum na vituo vya kulelea watoto yatima kwa lengo la kuunga mkono jitihada za serikali za kuwasaidia watu wenye uhitaji ili kuwafariji na kuwatia moyo.’Alisema Samasuba.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo Mwakilishi wa kituo cha kulelea yatima  cha Mchungaji mwema cha Mjimwema Sr. Maria Veronika OSB ,ameishukuru Kampuni hiyo kwa msaada huo ambao amesema utawasaidia watoto 39 ambao wanalelea na kituo hicho.

Naye Mwakilishi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha SWACCO Castrol Whero amesema kitendo kilichofanywa na Mohamed Enterprise kimeleta faraja kubwa kwa sababu yatima ni kundi maalum lililopo katika jamii linalohitaji msaada.

Amesema kituo cha SWACCO kilianza mwaka 2000 kikiwa na watoto 50 ambapo hivi sasa kituo hicho kinalea watoto 23 na watoto 31 wanahudumiwa wakiwa majumbani na walezi wao.

Vinsent Ndumbaro ni Kaimu Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Ruvuma akizungumza kwa niaba  ya serikali,ameipongeza na kuishukuru Kampuni ya Mohamed Enterprise kuunga mkono juhudi za serikali za kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum ambapo ametoa rai kwa wadau wengine kuiga mfano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...