Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Mbopo kata ya Mabwepande wilaya ya Kinondoni, Mohamed Bushir akizungumza na wazazi,walezi  leo  tarehe 4 Februari 2021.  katika mkutano  wa kujadili masuala mbalimbali kuhusina na maendeleo ya shule, mkutano  ulifanyika katika shule ya Sekondari  ya Njechele  ambapo ameziomba mamlaka za juu kusaidia umaliziaji wa bweni la wanafunzi  wa kike ambao wanatoka maeneo mbalimbali ya jijini Dar es Salaam kuja kusoma katika shule hiyo ambayo imekuwa ya nne kwa wilaya ya Kinondoni kwenye matokeo ya kidato cha nne.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Mbopo kata ya Mabwepande wilaya ya Kinondoni, Mohamed Bushir akiwa ameambatana na wazazi na walezi baada ya mkutano kumalizika wakikaguwa jengo la bweni ambalo halijakamilika kwa kukosa vitanda uzio na vitu mbalimbali leo  tarehe 4 Februari 2021. Jijini Dar es Salaam.
Mwalimu Mkuu  wa Shule ya Sekondari ya Njechele,Dickson Kajuna akizungumza na Michuzi Tv ambapo amesema shule yake imekuwa ya nne kiwilaya kwenye matokeo ya kidato cha nne na endapo mabweni yakikamilika shule hiyo itakuwa ya kwanza  kwakuwa wanafunzi wa kike  hawatasafiri umbali mrefu,  leo  tarehe 4 Februari 2021. Jijini Dar es Salaam.

Muonekano wa Jengo la Mbweni la Shule ya Sekondari Njechele kata ya Mabwepande wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Wazazi na walezi wakimsiliza Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Mbopo kata ya Mabwepande wilaya ya Kinondoni,Mohamed Bushir.(Picha na Emmanuel Massaka, Michuzi TV.)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...