NA  YEREMIAS  NGERANGERA…..NAMTUMBO.

Mwenyekiti  wa chama  cha mapinduzi  wilayani  Namtumbo  mkoani Ruvuma bwana  Aggrey  Mwansasu  alitumia  siku ya  maadhimisho ya miaka 44 ya kuzaliwa  chama cha mapinduzi  na kuwasisitizia viongozi  wa  vijiji  kufuata  utaratibu  wa  uingizaji wafugaji na mifugo  yao katika  maeneo  ya vijiji.

Mwansasu  alidai vitendo vinavyofanywa na baadhi  ya viongozi wa vijiji  kuwaingiza wafugaji kinyemera  bila kuwashirikisha wananchi  kupitia mikutano ya hadhara  kitasababisha  migogoro  kati ya  wakulima  na wafugaji  siku za usoni .

Mwenyekiti  wa  chama huyo  alitaja  kifo  cha kijana  Mohamedi  Athumani  Kinunga  kijiji  cha Matepwende  aliyekutwa  amekufa  porini  ni dalili zinazoanza kujionyesha  za kuwapokea  na kuweka  urafiki  na  watu wasiowajua  na waliopokelewa  kinyemera  bila kufuata  taratibu zilizowekwa na serikali alisema  mwenyekiti huyo.

Bwana  Mwansasu  pia aliwataka  viongozi  waliochaguliwa kuacha kutumia nafasi  walizopata  kwa kupoteza muda mwingi kupanga safu zao  kwa kuwatengenezea mazingira  viongozi  waliopo katika madaraka  waondolewe  waweke  viongozi  wengine wanaowataka  kwa  kutumia muda mwingi  kufanya shughuli  hiyo  badala ya  kuwaletea wananchi maendeleo.

Naye  Mbunge  wa jimbo  la Namtumbo  mheshimiwa  Vitta  Rashid  Kawawa  alianza  kwa kuwashukuru  wananchi  kwa  kukipatia ushindi  wa kishindo  chama cha Mapinduzi  katika  uchaguzi mkuu  uliofanyika  mwaka jana oktoba  2020.

Hata  hivyo  Kawawa  aliwaomba wananchi  ushirikianao  katika utekelezaji wa  miradi, huku akisisitiza kumalizia miradi yote viporo  iliyoanzishwa  na wananchi kwa   kipindi  kilichopita na kuanzisha miradi mingine mipya .

Mohamedi  Mavallah  katibu  wa chama cha mapinduzi  wilaya ya Namtumbo  pamoja na  mambo mengine aliwasisitizia waheshimiwa  madiwani katika kata  zao kupanga ratiba  za  kusikiliza  kero  za  wananchi  katika kata  zao  na kuzitatua .

Abdulahamani  Milanzi (Jangala) mkazi wa  kijiji  cha Ulamboni  kata ya  Lisimonji  katika shairi  lake kwa mwenyekiti wa chama cha mapinduzi  wilaya ya Namtumbo  aliomba ujenzi wa  daraja  la mto Lukimwa litakalounganisha kata hiyo na kata ya Lusewa, kutengenezewa   barabara  zakuunganisha  vijiji  kata hiyo ziweze  kupitika muda wote ,

Maadhimisho  ya  kumbukumbu  ya kuzaliwa  chama cha mapinduzi  miaka 44 iliyopita yalifanyika  kiwilaya kijiji cha Matepwende tarehe  3mwezi huu  katika kiwanja  kilichojengwa  mnara  wa kumbukumbu  ya  asili ya  Hayati Rashid Mfaume  Kawawa aliyekuwa  Waziri Mkuu wa serikali ya Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...