Na Pamela Mollel,Arusha

Mawakili kutoka chama cha Mawakili Tanganyika TLS wamejitokeza kuaga mwili wa wakili na mwanachama wa siku nyingi wa chama hicho Loomu Ojare aliyefariki ghafla hivi karibuni

Mwenyekiti wa chama cha mawakili wa kujitegemea Kanda ya Arusha Elibariki Maeda akiwaakilisha TLS katika ibada ya kumuaga Ojare alisema wakili Ojare atakumbukwa kwa tendaji kazi  mzuri na ushirikiano aliokuwa nao na mawakili wenzake

Maeda alisema Ojare alikuwa mchapakazi na mwenye kujituma ikiwemo kuwasaidia watu waliohitaji msaada wa kisheria bure kwa kuwa hakupenda kuona mtu akionewa

" sisi kama mawakili tuliomkuta Ojare Kazini tulijifunza mambo mengi kutoka kwake alituelekeza pasipo kuchoka na alikuwa mtu aliyependa haki"Alifafanua Maeda

Kwa upande wake Kaimu Msajili wa Mahakama kuu  Kanda ya Arusha John Nkwabi akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya serikali alisema Marehemu Ojare alikuwa akilea na kuwafundisha vijana wengi kwenye taaluma ya Sheria hivyo kuondoka kwake ni pigo kwa serikali na Taifa kwa ujumla

Nkwabi alisema  Marehemu Ojare alikuwa mtu aliyependa haki na hakutaka kumwona mtu akidhulumiwa haki yake na kuwataka mawakili waliobaki kuiga Mfano wa Marehemu kwa kuendeleza kazi nzuri iliyoachwa na Ojare

Mchungaji kiongozi wa Kanisa la KKKT Usharika wa Elkyurei  Daniel Thimothi akiongoza ibada ya mazishi ya Marehemu Ojare alisema kuondoka kwa Ojare ni pigo si tu kwa jamii inayozunguka ila pia kwa kanisa hilo kwani alikuwa kiongozi wa Kanisa

 "Marehemu alikuwa kiongozi wa kanisa na ujenzi wa kanisa hili yeye alikuwa wanakamati katika kamati ya ujenzi hivyo kanisa limepata pigo kubwa"Alisema Mchungaji Thimothi.

Awali akisoma risala ya Marehemu mtoto wa marehemu Diana Ojare  alisema marehemu baba yake alifariki ghafla kwa kuwa hakuumwa kwa muda mrefu na kwamba siku ya kufariki marehemu Ojare alikuwa ofisini akihudumia wateja na baadae alijisikia vibaya na alipokimbizwa hospitali alifariki dunia

Diana alisema wao kama Familia kifo cha baba yao kimewaachia pengo kubwa kwa kuwa alikuwa msaada mkubwa kwao na tegemezi Kwa familia na hivyo kutoa shukrani kwa watu wote walioshiriki katika kumpumzisha baba yao

Marehemu Loomu Ojare alizaliwa mwaka 1952  na alifanya kazi kama wakili wa serikali kwa kipindi kirefu kabla ya kuachana na kazi za serikali na kujiajiri kama wakili wa kujitegemea mwaka 1983

Aidha Marehemu ameshiriki katika kazi mbalimbali za uwakili ambapo hadi umauti unamkuta alikuwa mwanachama wa chama cha mawakili Tanganyika (TLS) na mwanachama wa Club ya mawakili Arusha na ameacha watoto wanne.

Sehemu ya mawakili wakibeba jeneza la Loomu Ojare kutoka kanisan kuelekea nyumbani kwake kwaajili ya maziko
Watoto wa marehemu, wakili Loomu Ojare wakiongoza msafara wa waombolezaji kutoka kanisa la KKKT Olkiurei kuelekea nyumbani  kwa ajili ya mazishi
Wakili maarufu Tanzania, Loomu Ojare,enzi za uhai wake

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...