Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV

Mkazi wa Tabora - Sikonge, ambaye ni Maajiriwa wa Duka la Dawa na Maabara, Abdulaziz M. Ibrahim (24) amejishindia kitita cha Shilingi 521,471,360/- alichoshinda katika Jackpot ya Mechi 13 akiwa Mshindi wa awamu ya Sita wa Jackpot hiyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi SportPesa, Abbas Tarimba amesema mshindi huyo wa Jackpot ya Mechi 13 atakabidhiwa kitita cha Shilingi 417,177,488/- na atalipa Kodi ya Shilingi 104,293,872/-

Tarimba amesema ili Wachezaji wa Jackpot hiyo washinde ilikuwa lazima watabiri matokeo yote 13 ya michezo hiyo kwa usahihi kwa matokeo yanayotokea uwanjani.

Kwa upande wake, Mshindi wa Jackpot hiyo, Abdulaziz M. Ibrahim amesema ushindi huo alioupata kupitia Jackpot hiyo ana malengo ya kujenga Msikiti, amesema hana maelngo ya kupata jiko kwa sasa hivyo atatumia pesa hiyo kwa masuala mengine.

 Wachezaji wa Young Africans, Farid Mussa, Bakari Mwamnyeto, Carlos Carlinhos na Mchezaji wa Simba SC, Miraji Athuman wakimkabidhi mfano wa hundi Mshindi wa awamu ya Sita wa Jackpot ya Sportpesa, Abdulaziz M. Ibrahim (24) alijishindia kitita cha  
Shilingi 521,471,360/-

2 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi SportPesa, Abbas Tarimba akimkabidhi Mshindi mfano wa Hundi yenye kiasi hicho cha fedha.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...