KATIKA Kuimarisha utendaji kazi na kuleta tija kwa jamii na Serikali Naibu Waziri na Ujenzi na Uchukuzi Mwita Waitara  amekutana na Menejimenti za Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo Mkoani Dar es Salaam na kujadili ubireshaji wa Wizara hiyo.

Katika kikao hicho,  Waitara amepata nafasi ya kupokea taarifa mbalimbali za utekelezaji kutoka katika Taasisi hizo.

Aidha, Waziri Waitara amezitaka taasisi hizo kufanya kazi kwa weledi na ubunifu ili kuiwezesha Serikali kupata mapato ambayo yatasaidia katika utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini.

 Aidha ameahidi kutembelea kila taasisi ili kujadiliana kwa kina juu ya utekelezwaji wa   majukumu, changamoto, mafanikio na mikakati ya kusonga mbele katika kutekeleza majukumu ya wizara.

Vilevile Waitara amezitaka menejimenti zote kuipitia upya hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipolihutubia Bunge na watanzania wote Aprili 22, 2021 ili kuyachambua maono ya Mhe. Rais na kujipanga vizuri kuyatekeleza.

Mkutano wa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Mwita Waitara na menejimenti za Taasisi ni mkutano wa kwanza tangu Mhe. Waitara alipoteuliwa na kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kushika nafasi hiyo.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...