Gari iliyobeba mwili wa hayati askofu wa jimbo la Njombe ukitoka uwanja wa ndege mara baada ya kuupokea mwili huo uliowasili leo mchana kutokea jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya mapadre mkoani Njombe wakiupokea mwili wa hayati askofu wa jimbo la Njombe kutoka kwenye ndege ulipowasili ukitokea Dar es Salaam.
Mwili wa askofu Maluma ukiwa kwenye jeneza mara baada ya kushushwa uwanja wa ndege ukiombewa tayari kwa kupelekwa kanisani.
Baadhi ya wananchi wakiwa barabarani kushuhudia maandamano mara baada ya kupokea mwili wa askofu Maluma wa jimbo la Njombe.
Kati kati aliyevaa miwani myeupe ni mzee Philip Mangula makamu mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM Tanzania bara na wakwanza kulia ni mkuu wa mkoa wa Njombe Mhandisi Marwa Lubirya wakiwa kanisani wakati wa kuaga mwili wa askofu Maluma katika kanisa katoliki jimbo la Njombe
Kati kati aliyevaa barakoa ni mbunge wa jimbo la Njombe mjini Deodatus Mwanyika wakiwa kanisani wakati wa kuaga mwili wa askofu Maluma.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...