Na Amiri Kilagalila, Njombe
Msongamano
wa wafungwa kwenye gereza kuu la mkoa wa Njombe (mpechi) umekuwa
kikwazo kikubwa katika utendaji kazi za kila siku katika gereza hilo.
Hayo
yameelezwa leo na mkuu wa gereza hilo mkoa wa Njombe, Emmanuel Lwinga
katika uzinduzi wa bodi ya Parole ya mkoa huo uliofanyika mkoani hapa.
Amesema
gereza hilo lilipaswa kuwa na wafungwa wasiozidi 100 lakini kwasasa
kuna wafungwa 300 hali inayosababisha gereza hilo kuwa na msongamano
mkubwa.
Amesema kutokana
na wilaya ya Wanging'ombe kutokuwa na gereza hivyo wafungwa wote wa
wilaya wanapelekwa katika gereza la mkoa na kusababisha wafungwa kujaa
katika gereza hilo.
Amesema
kupitia sheria ya Parole itasaidia kupunguza msongamano gerezani
kwasababu sheria hiyo inaruhusu wale wenye vigezo ambao wamefungwa zaidi
ya miaka minne kunufaika na sheria hiyo.
Amesema
mchako wake unaanzia gerezani kwa kupendekeza jina la mfungwa kisha
kwenda katika kijiji anachotoka mfungwa huyo kwa ajili ya kuchunguza.
"Yule
aliyefanyiwa kosa anahojiwa kama wanaweza kumpokea na akikubali
mapendekezo yanapelekwa bodi ya mkoa na bodi hiyo inapeleka ngazi ya
taifa na baadae kwa waziri," amesema Lwinga.
Amesema
wanufaika wa sheria hiyo ni wale wenye makosa madogo isipokuwa ya
yanayohusiana na ubakaji na uhalifu wa kutumia silaha, hawahusiki na
msamaha huo.
Mkuu wa Mkoa
wa Njombe, Mhandisi Marwa Rubirya ambaye alikuwa mgeni rasmi katika
uzinduzi huo uliofanyika gerezani hapo amesema malengo ya kuanzishwa
bodi ya Parole ni kupunguza changamoto kubwa ya msongamano wa wafungwa
katika magereza.
Amesema
bodi hiyo itasaidia kupitia orodha ya baadhi ya majalada ili kuona
uwezekano wa kupunguza msongamano kwa baadhi yao kuachiwa chini ya
sheria hiyo.
"Lengo la pili ni kushirikisha jamii katika suala zima la urekebishaji wa tabia kwa wale wanaokutwa na hatia" amesema Rubirya.
Baadhi
ya wajumbe wa bodi hiyo akiwemo Sheikh wa Mkoa wa Njombe, Rajabu Msigwa
na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi
ya Kusini, George Fihavango wamesema jamii inapaswa kujifunza kusamehe
kwakuwa kila mmoja ni mkosaji mbele ya mungu.
"Katika
mazingira ya kidini hata sisi huwa tunamkosea muumba wetu na yeye huwa
anatusamehe, anasema nipo tayari kuwasamehe waja wangu pindi
wanaponiomba msamaha," amesema Rajabu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...