WAZIRI wa Viwanda na Biashara Prof Kitila Mkumbo  amewataka Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo kufanya kazi kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu  zinazotumika kusimamia taasisi hizo na sikuwa kikwazo katika kutoa huduma  bora kwa wananchi. 
Waziri  Mkumbo  aliyasema hayo alipokuwa akitoa mwelekeo wa utekelezaji wa majukumu ya Wizara katika kikao na Wakuu wa Taasisi hizo  kilichofanyika  tarehe 09/04/2021 katika ukumbi wa Chuo cha Biashara jijini  Dodoma. 
“Taasisi zote zilizochini ya Wizara ya Viwanda zinamchango mkubwa katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara hivyo nawasihi muendelee kufanya kazi kwa mujibu wa Sheria Kanuni na taratibu zinazosimamia taasisi zenu katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi na si kuwa kikwazo”  Amesema Waziri Mkumbo.
Aidha, Wakuu wa Taasisi waliohudhuria kikao hicho kutoka TBS, WMA, BRELA, TANTRADE, SIDO, NDC, EPZA, FCC, FCT, WRRB, TIRDO, CAMARTEC, TEMDO na CBE walipata fursa ya kutoa maoni na changamoto mbalimbali zinazozikabili taasisi hizo katika utekelezaji wa majukumu yake kwa Waziri wa Viwanda na Biashara.
Waziri Mkumbo ameahidi kuendelea kupokea ushauri wa kitaalamu kutoka katika taasisi hizo pamoja na kutatua changamoto mbalimbali zinazozikabili taasisi hizo katika utekelezaji wa majukumu yake ikiwemo upatikanaji Bodi zinazofanya kazi katika kila taasisi ili kurahisisha utoaji wa maamuzi sahihi na kwa wakati.
Naye Naibu Waziri akiongea na Wakuu wa Taasisi hizo, alisema kuwa mchango wa taasisi hizo  ni muhimu na zinategemewa katika kuifanikisha Wizara  kufikia malengo ya taifa katika ukuaji wa viwanda na biashara shindani na hivyo kukuza uchumi wa nchi.
Waziri wa Viwanda na Biashara 
Prof. Kitila Mkumbo (Mb) akitoa mwelekeo wa utekelezaji wa majukumu ya 
Wizara  alipokutana na Wakuu wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara katika 
kikao kilichofanyika  tarehe 09/04/2021 katika ukumbi wa Chuo cha 
Biashara jijini  Dodoma. 
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani Dkt John Mduma akitoa maoni kuhusu ukamilishaji wa mapitio mbalimbali ya Sera na Sheria zinazosimamia taasisi zilizopo chini ya Wizara ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi kwa Mhe. Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo katika kikao na wakuu wa taasisi hizo kilichofanyika tarehe 09/04/2021 katika ukumbi wa Chuo cha Biashara jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Mhandisi Prof. Sylvester Mpanduji akitoa maoni kuhusu uboreshaji wa huduma zinazotolewa na SIDO kwa Mhe. Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo katika kikao na Wakuu wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara kilichofanyika tarehe 09/04/2021 katika ukumbi wa Chuo cha Biashara jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Naibu Waziri wa
 Viwanda na Biashara Bw. Dotto James akifafanua jambo katika Kikao cha 
Wizara na Wakuu wa Taasisi zake Kikao hicho kilicholenga kujadili 
mwelekeo wa utekelezaji wa majukumu ya Wizara kilifanyika  tarehe 
09/04/2021 katika ukumbi wa Chuo cha Biashara jijini  Dodoma. 
Waziri wa Viwanda na Biashara 
Prof. Kitila Mkumbo (Mb) akitoa mwelekeo wa utekelezaji wa majukumu ya 
Wizara  alipokutana na Wakuu wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara katika 
kikao kilichofanyika  tarehe 09/04/2021 katika ukumbi wa Chuo cha 
Biashara jijini  Dodoma. 
Kushoto ni Kaimu Afisa 
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA) Bi. Stella Kahwa, Katikati ni 
Mrajis wa Baraza la Ushindani Bw Renatus Rutatinisiwa akifuatiwa na  
Kaimu Mkurugenzi Mkuu waa  NDC Bi Rhobi Sattima wasilikiliza maelekezo 
ya Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo  katika kikao na 
Wakuu wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara kilichofanyika  tarehe 
09/04/2021 katika ukumbi wa Chuo cha Biashara jijini  Dodoma. 
Naibu Waziri wa Viwanda na 
Biashara Mhe. Exaud Kigahe (Mb) (kulia) akiwa na Naibu Katibu Mkuu wa 
Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt  Hashil  Abdallah (kushoto) wakiwa 
katika Kikao  cha Wizara na Wakuu wa Taasisi zake. Kikao hicho 
kilicholenga kujadili mwelekeo wa utekelezaji wa majukumu ya Wizara 
kilifanyika  tarehe 09/04/2021 katika ukumbi wa Chuo cha Biashara 
jijini  Dodoma




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...