Na Mwandishi wetu, Babati


MWENDESHA mashtaka wa Mkoa wa Manyara, Mutalemwa Kishenyi anashikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoa wa Manyara, kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya shilingi milioni tano.

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara, Holle Joseph Makungu ameyasema hayo Mjini Babati wakati akizungumza Aprili 25, mwaka huu.

Makungu amesema kwamba Mwendesha mashtaka huyo wa Mkoa wa Manyara, wakili  Kishenyi amekamatwa  Aprili 23 mjini Babati usiku akiwa anapokea  kiasi cha shilingi milioni tano kwa watuhumiwa wa makosa ya jinai.

Amesema watuhumiwa hao walikamatwa katika upekuzi uliofanywa na mamlaka za dola  ambapo walikamatwa  na risasi 370 na stika bandia zenye thamani ya shilingi bilioni sita.

Mkuu huyo wa TAKUKURU amesema kuwa Mwendesha mashtaka huyo alikamatwa wakati akipokea rushwa ili kuwasaidia watuhumiwa hao.

"Uchunguzi zaidi wa tuhuma hizi unaendelea na ukikamilika mtuhumiwa huyu atafikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma husika," amesema Makungu.
 
 Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara, Holle Joseph Makungu akizungumza na waandishi wa habari Mjini Babati.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...