Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Daniel Chongolo jioni ya leo tarehe 30 Aprili, 2021 ameripoti Ofisini na kuendesha kikao maalum cha utambulisho kwa Wajumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa katika  Ofisi za Makao Makuu ya Chama Dodoma.

Pamoja na wajumbe wengine wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), Kikao hiko kimehudhuriwa na Wajumbe wapya akiwemo Naibu Katibu Mkuu - Bara Ndg. Christina Mndeme na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Itikadi na Uenezi Ndg. Shaka Hamdu Shaka.

Kikao hiko maalum cha utambulisho, pia kimejumuisha viongozi wastaafu wakiongozwa na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM -  Bara Ndg. Rodrick Mpogolo na aliyekuwa Katibu wa NEC, Oganaizesheni  Ndg. Pereira Silima.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...