Waziri wa
Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo
amesema Serikali kwa kushirikiana na mamlaka husika itaandaa Mkakati wa
udhibiti wa athari za zebaki kwa afya ya binadamu na mazingira.
Jafo
amesema hayo leo Aprili 27 wakati akiwasilisha Hotuba ya Mapato na
Matumizi kwa mwaka wa fedha 2021/2022 bungeni jijini Dodoma.
Alisema
sambamba na hayo itaainisha na kufanya tathmini ya maeneo yenye
shughuli nyingi za uchimbaji mdogo wa dhahabu kwa kutumia zebaki na
kuweka mikakati ya kuyarejesha katika hali yake ya asili.
Aidha,
waziri huyo aliongeza kuwa katika kutekeleza Mpango-kazi wa Taifa wa
kupunguza matumizi ya zebaki kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu nchini
Serikali itatoa mafunzo kwa mamlaka zinazohusika na udhibiti wa zebaki
kuhusu namna ya kudhibiti uingizaji, matumizi na utupaji wa taka
zitokanazo na zebaki nchini.
Katika hotuba hiyo pia alisisitiza
kuwa Serikali itaendelea kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala kwa
kuandaa Mkakati wa Nishati Mbadala ya Kuni na Mkaa kwa ajili ya kupikia
na kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu matumizi ya nishati mbadala.
“Mheshimiwa
Spika tutaendelea kutoa elimu ya nishati mbadala hususan hususan kwa
taasisi zinazotumia kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia zikiwemo magereza,
polisi, na taasisi za elimu. Katika kipindi hiki, Ofisi itaendelea na
ufuatiliaji wa utekelezaji wa mipango iliyowekwa na taasisi mbalimbali
kuhusu matumizi ya nishati mbadala,” alisema.
Kwa upande wake
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na
Mazingira Mhe. Eric Shigongo alishauri Ofisi ya Makamu wa Rais
ishirikiane na Ofisi ya Mkemia Mkuu kudhibiti uingizwaji wa zebaki
nchini.
Katika hotuba hiyo aliyoiwasilisha kwa niaba ya
Mwenyekiti Mhe. David Kihenzile alishauri Serikali itafute teknolojia
mbadala ambayo wachimbaji hao wataitumia ili kuachana na matumizi ya
zebaki.
“Uingizaji holela na utumiaji wa kemikali ya Zebaki
nchini kutokana na kuwapo kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu wanotumia
kemikali hiyo, unaathiri kwa kiasi kikubwa afya na usatwi wa wchimbaji
hao. Madhara ya matumizi ya kemikali hiyo yanatokana na wachimbaji wengi
kuitumia bila ya kuwa nyenzo za kujinga kutokana na zebaki,” alisema.
Shigongo
ambaye pia ni Mbunge wa Buchosa alitahadharisha kuwa maji yanayotumika
kusafishia dhahabu yakiwa yamechanganyika na Zebaki, yanatiririkia
kwenye vyanzo vya maji na kuwa watu wanapotumia maji hayo.
Naye
Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Hawa Mchafu alishauri Serikali itumie fedha
kutoka mifuko ya mazingira kwa kusaidia katika kujenga uelewa wa
kupunguza matumizi ya zebaki.
Pia Mbunge huyo alipendekeza njia
mbadala ya matumizi ya zebaki na kusema kuwa kemikali hiyo ina athari
kubwa kwa binadamu hususan katika maeneo ya Kanda ya Ziwa ambako kuna
shughuli za uchimbaji wa dhahabu.
6.6 Matumizi ya kemikali hatarishi – Zebaki
Mheshimiwa
Spika, uingizaji holela na utumiaji wa kemikali ya Zebaki nchini
kutokana na kuwapo kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu wanotumia kemikali
hiyo, unaathiri kwa kiasi kikubwa afya na usatwi wa wchimbaji hao.
Madhara ya matumizi ya kemikali hiyo yanatokana na wachimbaji wengi
kuitumia bila ya kuwa nyenzo za kujinga kutokana na zebaki. Vilevile,
maji yanayotumika kusafishia dhahabu yakiwa yamechanganyika na Zebaki,
yanatiririkia kwenye vyanzo vya maji kama vile mito na mawaziwa. Watu
wanapotumia maji kutoka vyanzo hivyo vilivyochafuliwa na zebaki ya
kuoshea dhahabu, huathirika kiafya na wakati mwingine kupata maradhi
sugu yanayogharimu maisha yao.
Mheshimiwa Spika, Kutokana na hali hiyo, Kamati inashauri kuwa:-
i) Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira ishirikiane na Ofisi ya Mkemia Mkuu kudhibiti uingizwaji na zebaki nchini;
ii) usimamizi na uratibu matumizi ya zebaki kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu nchini
25
uendelezwe na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa pamoja na Ofisi ya Mkemia Mkuu; na
iii) Serikali itafute teknolojia mbadala ambayo wachimbaji hao wataitumia ili kuachana na matumizi ya zebaki.
6.7 Taarifa ya Hali ya Mazingira nchini
Mheshimiwa
Spika, Kifungu 175 (1) cha Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004 kinamtaka
Mkurugenzi wa Mazingira kuandaa na kutoa taarifa juu ya Hali ya
Mazingira nchini kila baada ya miaka 2 na kuiwasilisha Bungeni. Hata
hivyo uzoefu unaonesha kuwa upo ugumu wa kutekeleza masharti hayo jambo
lililosababisha kuwasilishwa kwa taarifa hiyo mwaka 2008, 2014 na 2019.
Kwa sababu hiyo, taarifa ya kwanza, ya pila na ya tatu hazikuweza
kuzingatia masharti ya kuwasilishwa baada ya miaka miwili. Kwa msingi
huo, Kamati inashauri kuwa Serikali iandae mapendekezo ya marekebisho ya
kifungu hicho kwa kuongeza muda wa kutoa ripoti kufikia miaka 5.
Home
HABARI
Waziri Jafo awasilisha Hotuba ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2021/2022 bungeni jijini Dodoma
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...