NA FARIDA SAIDY, MOROGORO.


Vijana wametakiwa kuzingatia tabia chanya za usafi katika maeneo hayo ikiwemo kunawa mikono,kutumia maji safi pamoja na kudhibiti kusambaa kwa taka ngumu katika maeneo yao hali itakayosaidia kutunza na kulinda mazingira.
 
Wito huo umetolewa  wakati wa kampeni ya KIJANA NI USAFI ambayo inalenga kuhamasisha tabia ya usafi kwa vijana wakitanzania inayosimamiwa na Shirika la Raleigh Tanzania chini ya ufadhili wa   shirika  la msaada wa Uingereza( UKAID).
 
Kampeni hiyo itakayodumu ndani ya miezi 6 inawalenga vijana wa wakike na kiume wenye umri wa miaka kati ya 15-35,ambapo inatarajia kufikia zaidi ya vijana 48,000 katika mikoa ya minne ambayo ni Iringa,Morogoro,Dodoma na Dar es salaam. 
 
Akizungumza katika kampeni hiyo Mratibu wa Mradi,Bwana Augustino  Dickson amesema kampeni hiyo katika Manispaa ya Morogoro itajikita katika itahimiza matumizi ya maji safi na salama,na kuitaka jamii kuacha kuishi kwa mazoea.
 
Hata hivyo ameongeza kuwa Mkoa wa Morogoro unaathiwa na Magonjwa ya mlipuko ya mara kwa mara ya kiwemo mlipuko wa ugonjwa wa  Kipindupindu hali ambayo inatokana na  jamii kutotumia maji safi na salama.
 
Aidha ameongeza kuwa kampeni ya KIJANA NI USAFI itaendelea kulenga kundi la vijana kwa sababu vijana ndio kundi lenye idadi kubwa ya watu Nchini, huku akiongeza kuwa vijana wanaweza kuwa wakala wa mabadiliko chanya katika jamii endepo watajengewa uwezo kuhusu elimu ya mazingiara. 
 
Katika kampeni mafunzo mbalimbalia ya namna ya kuhifadhi maji safi na salama yametolewa kwa wananchi,huku wakazi wa Manispaa ya Morogoro wakilishukuru Shirika la Raleigh Tanzania kwa kuwapatia elimu ya mazingira.

 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...