NA YEREMIAS NGERANGERA…NAMTUMBO.

Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo mkoani  Ruvuma imeuza kilo  529,758 za  zao la ufuta kwa mfumo wa  stakabadhi ghalani katika soko la kwanza  katika chama  cha ushirika  NAPPACOS  kwa  msimu wa mwaka 2020/2021.

Mwenyekiti  wa kamati ya stakabadhi  ghalani ambaye  pia ni afisa kilimo ,ushirika na umwagiliaji  bwana  joseph  Mbilinyi  alisema zaidi ya kilo 529,758  za  ufuta zimeuzwa  kwa mfumo wa stakabadhi ghalani kwa mnunuzi  mmoja kampuni ya AFRISIAN GINNING LIMITED  kushinda mnada huo kwa bei  ya shilingi 2,282 kwa kilo..

Kwa  mujibu wa mwenyekiti huyo  alidai makampuni 7yalijitokeza  kwenye  mnada kutaka  kununua ufuta huo kwa njia ya  mnada ni Afrisian Ginning Limited shilingi 2,282, Hs implex limited shilingi 2,150,Sm Holding limited shilingi 2,221,Yihay Kerry limited shilingi 2,100.

Makampuni mengine ni  RBST International limited shilingi 1,800 Mohamed enterprises Limited shilingi 2,150 na kampuni ya Export Trading Limited  iliyopanga kununua ufuta huo kwa njia ya mnada kwa shilingi 2,024.

Mwajuma  Ngonyani mwanachama wa chama cha msingi cha Mihagambo kilichopo katika kijiji cha Nangero pamoja na  kuishukuru serikali  kwa kuanzisha mfumo wa stakabadhi ghalani  aliiomba serikali hiyo kuboresha maghala yaliyopo katika kata zao ili waweze  kwenda kuhudhuria minada kutokana na hali ngumu ya kiuchumi waliyonayo wakulima wengi na kuamua bei ya mazao yao badala ya watu waliokuwa karibu na maghala au wenye uwezo wa kusafiri umbali mrefu ndio watakaoamua bei ya mazao yao..

Kupitia  mnada huo  vyama vya msingi vya ushirika  vilivyopo katika  wilaya ya Namtumbo vitapata kiasi cha shilingi 1,162,818,810  kupitia  vyama  vyao  baada ya kutoa makato ya shilingi 87 kwa kilo  kwa wakulima kadiri ya makubaliano ya kwenye  kikao cha wadau wa stakabadhi ghalani kilichofanyika  katika ukumbi wa Halmashauri ya Namtumbo hivi karibuni.

Halmashauri  ya wilaya ya Namtumbo kwa mnada huo wa awali mzunguko wa  fedha  utakuwa wa shilingi  1,208,907,756 ikiwa  malipo ya vyama vya msingi  shilingi 1,162,818,810  huku ushuru wa  Halmashauri  ya wilaya ya Namtumbo shilingi 30,196,202 na shilingi 14,833,224 kwa ajili ya mfuko wa maendeleo  ambapo  kwa  sasa kila jumatano ya kila wiki kutakuwa na mnada wa zao hilo la ufuta.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...