Wizara
ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo inatarajia kuwakutanisha Maafisa
Utamaduni na Michezo lengo ikiwa ni kujadili mikakati bora ya
kuendeleza sekta hizo.
Akizungumza
Mei 06,2021 katika mahojiano na Kituo cha Redio cha A FM Jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo nchini, Yusufu Singo
ameeleza kuwa kikao hicho kitakua cha siku mbili na kitaongozwa na mada
mbalimbali pamoja na kujadili utekelezaji wa Sera,Kanuni na Miongozo
mbalimbali ya Sekta hizo.
Hata
hivyo, Mkurugenzi huyo alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa maandalizi ya
Mechi ya Simba na Yanga itakayochezwa Mei 08,2021 katika Uwanja wa
Benjamin Mkapa yamekamilika.
“Habari
na Michezo ni Sekta zinazotegemeana sana kwa mfano mwisho wa juma
hili tuna mechi ya Simba na Yanga, bila umma kuelezwa vizuri juu ya
mechi hii inaweza kukosa msisimko” amesisitiza Mkurugenzi Singo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...