Na Abdullatif Yunus Michuzi TV.

Mkuu wa Mkoa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti amewatakia Heri na fanaka Waislamu Mkoa Kagera katika Kuelekea Sikukuu ya Eid El Fitr.

Katika salaam hizo ambazo zimeambata na Mkono wa Eid, zimewasilishwa kwa Niaba yake na Katibu wa Mkuu wa Mkoa Bwn. Sylvesta Raphael alipokwenda kukabidhi zawadi hizo kwa Makundi Maalum.

Akikabidhi zawadi hizo ambazo Ni Mchele, Mafuta pamoja Kitoweo Cha Mbuzi, Bwn Sylvesta amesema Mkuu huyo ambae yupo katika Majukumu mengine ya kikazi, anawatakieni Waislamu Heri ya Sikukuu na anawapongeza kwa kuhitimisha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani salama, na kuwaomba washerehekee kwa Amani.

Akipokea Mkono wa Eid Sheikh wa Mkoa Kagera Haruna Kichwabuta amefurahishwa na namna Mkuu wa Mkoa anavyozidi kuwakumbuka Waislam hasa Makundi Maalum, na kwamba zawadi hizo zimekuja muda muafaka hivyo zitawafikia walengwa.

Zawadi zilizotolewa ni pamoja na Kilogramu 200 za mchele, Mafuta ya kula Lita 100 na Mbuzi watano. Tayari zawadi hizo zimekabidhiwa kwa Sheikh wa Mkoa Kagera, Makao ya Watoto Yatima wa Nusuru Yatima Kashai, pamoja na Makao ya Wazee Kiilima.






 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...