WASANII wakongwe nchini Juma Kassim Kiroboto almaarufu kwa  jina la Juma Nature na Chegge Chigunda wameuzindua wimbo wao leo unaokwenda kwa jina la 'Kucha' kwa kupitia kipindi Cha Traffic Jam kinachorushwa na Redio  Clouds.
Wakizungumza mara baada ya uzinduzi wa nyimbo hiyo ambao uko katika 'Audio' na  'Video'  Nature na Chegge wamesema huo ni mwanzo wa kuleta mambo mazuri kwa mashabiki wao ambao waliwakosa kwa kipindi kirefu.

"Ukituona ni kama tunafanana lakini Jambo ninaloweza kusema ni kwamba sisi ni wasanii wawili tofauti lakini tuna muunganiko mzuri kwenye ladha ya uimbaji" alisema Nature.
 
Naye Chegge amesema kuwa hivi sasa amerudi kivingine na pia yuko kwenye usimamizi maalumu hivyo wote   mmoja ana maneja wake ambao wanawasimamia katika kazi zao.
Aidha Mtangazaji wa kipindi  Cha Traffic Jam Gadner Habash almaarufu kwa jina la Captain alieleza umma ulikuwa katika uzinduzi huo uliofanyika katika eneo la nje ofisini hapo kuwa wimbo huo  umerekodiwa  na mtayarishaji  mchanga mwenye maskani yake Mkoani Iringa  aliyemtaja kwa jina la Halfan Yahya almaarufu kwa jina la  'Tizo Touch'.
Kutoka kushoto ni Mtangazaji wa Kipindi Cha Traffic Jum Gadner Habash akifuatiwa na msanii Juma Nature, Mtangazaji wa Traffic Jam Fetty na msanii Chegge Chigunda wakiwa katika picha ya pamoja mara baada uzinduzi wa wimbo wa Kucha  ulioimbwa  na kurekodiwa  kwa pamoja  na wasanii hao wakongwe  ambao katika miaka ya nyuma walitamba na makundi ya TMK Family na Wanaume Halisi.
Msanii wakongwe wa mziki wa Bongo Fleva Juma Kassim Kiroboto almaarufu kwa  jina la Juma Nature akifafanua jambo kwa waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa nyimbo wao leo unaokwenda kwa jina la 'Kucha' kupitia kipindi Cha Traffic Jam kinachorushwa na Redio  Clouds.
Wasanii wakongwe wa mziki wa Bongo Fleva Juma Nature na Chegge wakiingia katika Ofisi za Clouds Media wakati wa uzinduzi wa nyimbo wao leo unaokwenda kwa jina la 'Kucha'


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...