Wafanyakazi wa benki ya  I&M wakiwa na baadhi ya watoto walipotembelea kituo cha watoto yatima cha Lady Fatema kilichopo Mjimwema mageti saba, kigamboni Jijini Dar es salaam ambapo wametoa msaada wa vitu mbalimbali.
Timu ya benki ya I&M wakiwa katika picha baada ya leo Mei 11,2021 kutembelea kituo cha yatima chini ya mpango wao wa kujitolea wa 'IM for You'.
 

Na Mwandishi, Wetu

WAFANYAKAZI wa Benki ya I&M Tanzania wamejitolea msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo vyakula, nguo, sabuni pamoja na vifaa vya shule katika moja ya kituo cha kulea watoto yatima kiitwacho ‘Lady Fatema’  kilichopo Mjimwema Mageti Saba wilayani Kigamboni jijini Dar es salaam.

Wametoa msaada huo chini ya mpango wao wa ‘IM FOR YOU’ katika jitihada za kurudisha kwa jamii kupitia mpango huo ambapo wafanyakazi hujitolea kwa jamii kwa njia mbalimbali kama vile kutoa elimu ya fedha na ujasiriamali kwa wanawake na vijana ili waweze kujiajiri pamoja na kusaidia vitu mbalimbali kwa wahitaji.

Msaada huo umekabidhiwa leo Mei 11 mwaka 2021 kwa Wasimaizi wa kituo hicho Mariam Ramadhan na mmewe Kalekela Omari Mahmood walianzisha kituo hicho  mwaka 2011 wakiwa na lengo la kusaidia watoto yatima wanaoishi katika mazingira hatarishi wakiwapatia elimu, chakula na hifadhi ya kulala. 

Mbali na misaada mbalimbali inayopelekwa na wafadhili, kituo hicho kina changamoto ya eneo la kutosha kwa ajili ya kuhifadhi watoto wengi na wa jinsia tofauti kwani kwa sasa imewalazimu kubaki na jinsia ya kiume tu kutokana na ukosefu wa vyumba vya kutosha kwaajili ya watoto hao.

Katika kuadhimisha mwezi mtukufu wa Ramadhani na ikiwa ni wiki ya kuelekea sikukuu ya Eid Al-Fitr, wafanyakazi wa benki ya I&M waliamua kujitolea vitu hivyo katika kituo cha kulea watoto yatima Mjimwema Kigamboni ili na wao waweze kusheherekea na kufurahia sikukuu ya EID inayotarajiwa kuwa mwishoni mwa wiki hii kutegemeana na kuandama kwa mwezi.

Pia wafanyakazi wa benki ya I&M wametoa elimu ya usimamizi wa fedha na ujasiriamali kwa vijana na wanawake waliokuwa katika kituo hicho ili iweze kuwasaidia katika usimamizi wa fedha za kituo hicho pamoja na kujiajiri wao wenyewe pindi watakapoanza kujitegemea. 

Benki ya I&M kupitia wafanyakazi wake wameweza kufanya kampeni mbalimbali za kusaidia jamii kama vile kujitolea kwa kufundisha wanawake, vijana na wajasiriamali katika kikundi cha Wanawake wajasiriami kilichopo Yombo vituka, Temeke jijini Dar es salaam, vilevile wiki iliyopita wafanyakazi wa benki hiyo walijitolea damu  ili kusaidia wagonjwa wenye uhitaji wa damu katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...