wananchi watakiwa kuwaombea viongozi wa serikali pamoja naTaifa   hususani katika kipindi  hiki Cha mfungo wa Ramadhani ili amani iliyopo nchini iendelee kudumu .

wakizungumza viongozi wa dini wilayani Gairo mkoani Morogoro katika Dua  ya kuliomba  Taifa pamoja viongozi   wa serikali wamesema viongozi wanatakiwa kuombewa ili waweze kuongoza Taifa katika misingi yenye Amani na Upendo  ushirikino na kuwa na hofu ya Mungu .

Aidha kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Gairo Sirieli Nchembe amesema amani iliyopo nchini ni kutokana na viongozi waliopo madarakani pamoja na wananchi  wanayo hofu ya Mungu huku akawaomba wananchi hao kushirikiana katika shughuli zote za kulijenga Taifa na kuwaombea  wenye uwezo wa kutoa msaada waweze kutoa kwa watu wenye uhitaji Kama vile vyakula na misaada  mingine.

katika Dua ya Kuliombea Taifa  ilienda sambamba nakushiriki kwa futari iliyoandaliwa na mkuu wa Wilaya hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...