Na.Vero Ignatus.

ASKARI  wa Jumuiya ya Hifadhi za wanyamapori (WMA) wametakiwa kutumia   ujuzi wa kisayansi na teknolojia walioupata, ili kufanya  doria kwa kuzingatia na kuheshimu haki za binadamu pale wanapohisi kuna nyara za serikali.
 
Aidha  wametakiwa kutumia njia nzuri za ukamataji  na upekuzi, pale wanapohisi kuna eneo lina viashiria vya uwepo wa nyara za serikali.

Hayo yalisemwa jana  na Mkurugenzi wa Jumuiko la Maliasili Tanzania (TNRF),  Faustin Zacharia wakati wa kufunga mafunzo ya siku tatu, kwa askari 40 wa wanyamapori kutoka katika Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori za Enduiment na Lake Natron zilizopo wilayani Longido,  yaliyofanyika Bomang’ombe Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.

“Kweli malalamiko mengi kwa wananchi pale mnapohisi pana nyara za serikali mnaenda kuepkua watu bila kuzingatia haki za binadamu hili kaliangalieni sana katika utendaji wenu wa kazi,”alisisitiza.

Alisema  tangu mwaka jana Jumuiko la Maliasili Tanzania kwa ufadhili wa Mfuko wa Wanyamapori Duniani (WWF), linatekeleza mradi wa BMZ  wa mabadiliko ya tabia nchi, unaolenga kuondoa changamoto za mabadiliko hayo ili kuboresha  uhifadhi wa wanyamapori Tanzania.

Mwakilishi wa  Mfuko wa Wanyamapori Duniani (WWF) Prof. Noah Sitati  alisema mradi huu umewezesha kuwarudisha vijana wa jumuiya walishindwa kuendelea kutokana na janga la Corona ambalo limeathiri dunia kwasasa,,hivi sasa wamewezeshwa kulipwa ili kuendelea na shuguli zao. 

 Mbali na utoaji wa mafunzo hayo, pia Jumuiko la  TNRF  limekabidhi vifaa vya kufanya tathimini na kukusanya takwimu za wanyamapori, katika Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Enduiment, kwa ufadhili wa WWF.

 Alisema  vifaa hivyo ni simu janja za mkononi ,chaji ya mkononi (power bank), boksi  la maoni, hadubini na kifaa  kinachowezesha kupata mtandao  (Reuters ).

“Vifaa  hivi  tumetoa kwa lengo la kuboresha utendaji wa kazi zenu  katika maeneo mtakayoyafanyia  kazi,”alisema.
 
Mwenyekiti wa kamati ya usimamizi wa mradi wa Hifadhi ya Wanyamapori  Ziwa  Natron, Lee Olduka alisema mradi huo umekuwa na manufaa makubwa kwa wananchi na wanyamapori pamoja na mifugo, kwa kupata bwawa kubwa la maji.

Alishukuru kwa mafunzo hayo na vifaa walivyopata kwani vitaboresha utendaji kazi wao  na kutoa matokeo chanya.Meneja wa Hifadhi ya wanyamapori Enduiment  Peter Milanga alishukuru kwa teknolojia mpya ya mawasiliano ambayo itawasaidia katika majukumu yao ya ukusanyaji wa taarifa, kwani awali walikuwa wakifanya kazi hiyo kwa kutumia karatasi.

Kwa upande wao askari wa wanyamapori Juliana Paskali kutoka Hifadhi ya Wanyamapori Enduiment na Ismail Jacobu kutoka ziwa  Natron walisema mafunzo hayo  yamekuja wakati muafaka, ambapo itawaletea tija na matokeo chanya kwani yatawawezesha kufanyakazi kwa ufanisi.
 
Akizungumza kwa niaba ya serikali Ofisa  Wanyamapori wa Wilaya ya Longido Lomayani Saiguran alisema katika kulinda wanyamapori, rasilimali watu inahitajika hivyo uwepo wa askari wa Jumuiya za Wanyamapori waliowezeshwa wainaisaidia serikali kutoa huduma sehemu ambazo haiwezi kufika kwa wakati.
Askari wa WMAS Kama wanavyoonekana katika gwaride wakati wa kufunga mafunzo ya siku tatu, kwa askari 40 wa wanyamapori kutoka katika Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori za Enduiment na Lake Natron zilizopo wilayani Longido,  yaliyofanyika Bomang’ombe Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.
Mkurugenzi wa TNRF Faustine akiwa anafunga mazfunzo ya siku tatu kwa Askari wa WMA 
Picha ya washiriki wa mafunzo wakiwa ukumbini wakisiliza mada za mafunzo


 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 17, 2021

    Katika jambo ambalo halikutakiwa kabisa kufanya kiafya ni askari au mwanamichezo kuvaa barakoa. Tafadhalini acheni kuiga hovyo hovyo mambo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...