Na Mwamvua Mwinyi,Mafia
Mkuu
wa wilaya ya Mafia ,mkoani Pwani ,Eng.Martin Ntemo amekutana na kamati
ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi wilayani humo pamoja na kuzungumza na
watumishi na watendaji , kujitambulisha ambapo ametoa vipaombele vyake
ili kujiinua kimaendeleo.
Alisema
licha ya kupewa maagizo na mkuu wa mkoa wa Pwani ,Aboubakar Kunenge kwa
wakuu wa wilaya kwenda kusimamia migogoro mbalimbali ikiwemo ya ardhi
lakini pia atahakikisha anasimamia miongozo ya ilani ya chama cha
Mapinduzi na maendeleo ya wilaya kwa kutekeleza miradi kwa maslahi ya
jamii.
Atahakikisha
wilaya inakusanya mapato kikamilifu ili kuimarisha halmashauri hiyo na
kusisitiza kutenga asilimia 10 ya vikundi vya vijana ,wanawake na
walemavu.
"Mkabuni vyanzo
vipya vya mapato na kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato pasipo
kujisahau na vyanzo vya kizamani ambavyo vimezoeleka.
Akikabidhiwa
ofisi na mkuu wa wilaya aliyemaliza muda wake ,Nnduma ,Eng.Ntemo
aliwaeleza anashukuru kuona wilaya imeachwa salama anachoomba ni umoja
na ushirikiano ili kuyaendeleza mazuri yaliyoachwa na wengine.
Ameelezwa
zipo changamoto mbalimbali ikiwemo za kielimu upungufu wa madawati
,madarasa ,katika afya madawa ,hivyo atasimamia kuhakikisha zinapungua
kama si kumalizika kabisa.
Amejipanga
kuweka siku maalum ya kusikiliza kero za wananchi kwani itasaidia
kuzifikisha katika mamlaka husika na kuzipatia ufumbuzi.
Ntemo aliomba viongozi mbalimbali na watendaji kwenda na kasi ya serikali ya awamu ya tano na kumuunga mkono Rais wa sita Samia Suluhu Hassan ili kuifikisha Tanzania mahala pazuri zaidi Kiuchumi
Mkuu wa wilaya mpya Mafia Eng.Martin Ntemo akizungumza
jambo baada ya kukabidhiwa ofisi wilaya ya Mafia.(picha na Mwamvua
Mwinyi)
Mkuu wa wilaya mpya wa Mafia Eng. Martin Ntemo (kulia) akiwa katika
ofisi za CCM wilaya ya Mafia alipokutana na Kamati ya Siasa ya wilayani
humo. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM (W) Hassan Pango na kushoto ni
Katibu wa CCM Kulwa Milonge.(picha na Mwamvua Mwinyi) Mkuu wa wilaya ya Mafia aliyemaliza muda wake ,Shaibu
Nnduma akiongea wakati akimkabidhi ofisi Eng. Martin Ntemo.(picha na
Mwamvua Mwinyi)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...