Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

MAHAKAMA ya kikatiba nchini Afrika Kusini imemuhukumu aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Jacob Zuma kwenda jela miezi 15 baada ya kukutwa na hatia ya kutoshiriki vikao vya kamati maalum inayochunguza tuhuma zake za ufisadi na kujihusisha na rushwa alipokuwa madarakani.

Hukumu hiyo imetolewa leo na jaji Khampepe Sisi ambaye amesema, hukumu hiyo haitakuwa ya lazima iwapo Jacob Zuma atazingatia na kuheshimu maagizo ya mahakama na kuanza kuhudhuria vikao  vya kamati inayochunguza tuhuma za rushwa dhidi yake.

Awali Mwenyekiti wa kamati maalum inayochunguza tuhuma za Zuma, Raymond Zondo amekuwa akiiomba mahakama kumpeleke jela Zuma miaka miwili kwa kutoshiriki vikao vya kamati hiyo.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...