Na Jacqueline Liana, Lushoto

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Kanali mstaafu Ngemela Lubinga amewataka viongozi wa mashina ya Chama, katika wilaya za Lushoto na Mkinga mkoani Tanga, kuimarisha mashina ya CCM kwa kuongeza wanachama.

Akizungumza kwa nyakati tofauti akiwa katika ziara ya kutembelea mashina ya Chama katika wilaya hizo, Lubinga alitoa wito wa mashina kuimarishwa kwa kuongeza idadi ya wanachama, pamoja na kusimamia maendeleo.

Akifafanua alisema kwamba Chama hakiwezi kusonga mbele pasipo mashina kuwa imara.

"Kuongeza idadi ya wanachama wa CCM ni dhamana waliyo nayo viongozi wa Chama katika ngazi zote za uongozi," alisisitiza Lubinga.

Wajibu mwingine wa mashina ya CCM ni kuhakikisha kila kipengele cha Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025 inatekelezwa kwa maendeleo ya kila Mtanzania.

Alisema serikali inapeleka fedha nyingi katika Halmashauri kwa ajili ya kutekeleza miradi, hivyo CCM kilichounda serikali wanachama wake wanajukumu la kuhakikisha kila senti ya serikali inatumika kwa manufaa ya wananchi.

Aliwataka watumishi wa serikali kutimiza wajibu wao kwa umma kwa kutenda haki kwani kinyume chake ni dhambi.

"Kuwatendea haki watu ni wajibu wa msingi," alisema na kuongeza haki ikikosekana huweza kuzaa vurugu na migogoro pasipo sababu za msingi.

Aliwataka madiwani kuhakikisha fedha za serikali zinatumika inavyostahili ikiwa ni pamoja na kuboresha miradi ya huduma za jamii; afya, elimu, maji na barabara.

Mashina ambayo yametembelewa na Lubinga kuanzia Juni 12 hadi Juni 13, mwaka huu ni yaliyo katika kata za Duga, Mhinduro na Maramba wilayani Mkinga, pamoja na yale ya kata za Mlalo, Lushoto na Soni katika wilaya ya Lushoto.


MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Kanali mstaafu Ngemela Lubinga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...