Na Amiri Kilagalila,Njombe
BWENI la wasichana shule ya Sekondari Ikuwo wilayani Makete mkoani Njombe limeteketea kwa Moto huku ikisadikika chanzo chake kuwa ni hitilafu ya Umeme au mkaa ulioanzia Chumba cha Matron (Mlezi wa wanafunzi)

Moto huo ulioanza asubuhi leo majira ya saa moja umeteketeza vitanda vitanda, magodoro, nguo za wanafunzi pamoja na vifaa vyao huku wanafunzi wote wakiwa salama

Jumla ya thamani ya vitu vilivyoteketea bado haijajulikana huku tathmini ikiendelea kufanyika.

Kamati ya ulinzi na usalama Wilaya, Mkurugenzi mtendaji wilaya na wataalamu mbalimbali wamefika kuangalia mali zilizoteketea kwa Moto huo uliotokea
Chanzo:Kitulo FM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...