Awapa Somo la "MSHAHARA WAKO NI SAWASAWA NA MATUMIZI NA KUJIWEKEA AKIBA"
(Income = Consumption + Savings).

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amewataka Watumishi kukopa kwa malengo ya kuboresha maisha ya Sasa na baadae na kuhakikisha mikopo wanayochukuwa wanaitumia kuanzisha miradi yenye tija.

RC Makalla amewataka Walimu kuacha kurubuniwa kwa mikopo ya Chapu Chapu yenye riba kubwa ambayo mwisho wa siku inawaingiza Katika Maisha Magumu badala ya neema.

Aidha RC Makalla amewapatia Walimu somo la namna Bora ya kutumia Mshahara wao na kuweka akiba kwaajili ya kuanzisha miradi ya kujiimarisha kiuchumi ili watakapostaafu Waweze kuishi maisha Bora.

Hayo yote yamejiri wakati wa ufunguzi wa Semina ya Siku ya Walimu iliyoandaliwa na bank ya NMB.





 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...