Bwana Cosme Goundété (Benin) na Bi Keto Kayemba (Uganda) waliteuliwa kushika nafasi za Urais na Makamu wa Rais, mtawaliwa.
Hii ni mara ya pili NBAA kuhudumu katika Bodi ya PAFA kwa nafasi tofauti. Mnamo mwaka 2011, Mwenyekiti wa zamani wa Bodi ya Wakurugenzi ya NBAA, CPA Prof.Mussa Assad, aliteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa PAFA kwa miaka miwili na kisha kuwa Rais wa PAFA mnamo 2013 kwa miaka miwili, kabla ya kuachia nafasi yake baada ya kuteuliwa na Mhe. Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.
Kufuatia uteuzi huu Tanzania itanufaika kushiriki katika uundaji wa miongozo ya kawaida ya kiufundi, kimaadili na kielimu kwa taaluma ya uhasibu Afrika. Pia, kushiriki na kubadilishana taarifa na maboresho katika masuala ya kiufundi, mifumo ya udhibiti na kanuni za utawala bora wa Shirikisho. Kwa kuongezea, Tanzania itakuwa na jukwaa la kubadilishana habari muhimu juu ya taaluma ya uhasibu.
IMETOLEWA NA:
MAGRETH KAGEYA
AFISA MASOKO NA MAWASILIANO.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...