Afisa Elimu Msingi Kata ya Saranga wilaya ya Ubungo Mkoa wa Dar es salaam, Mwalimu Faustine Byalile (wapili kushoto) akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo leo kwenye maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyo fanyika katika viwanja wa shule hiyo.
Mkuu wa Shule ya Msingi King'ong'o Mwalimu, Fairuna Kidesu akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo pamoja na wahitimu wa kidato sita ambapo amewapongeza wahitimu haoa kwa moyo wao wa uzalendo wa kuwapatia wanafunzi wa shule hiyo mahitaji mbalimbali.
Wahitimu wa kidato cha Sita wakimkabidhi keki Afisa Elimu Msingi Kata ya Saranga wilata ya Ubungo Mkoa wa Dar es salaam, Mwalimu Faustine Byalile katikati ni Mkuu wa Shule ya Msingi King'ongo Mwalimu, Fairuna Kidesu.
Wahitimu wa kidato cha Sita wakikabidhi vifaa mbalimbali uongozi wa Shule ya Msingi King'ong'o iliyopo Kata ya Saranga Wilaya ya Ubungo mkoa wa Dar es salaam vyenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni Mbili.
Wahitimu wa kidado cha sita wakitoa taulo za kike kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi King'ong'o iliyopo Kata ya Saranga Wilaya ya Ubungo mkoa wa Dar es salaam leo kwenye maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika.
Afisa Elimu Msingi Kata ya Saranga wilata ya Ubungo mkoa wa Dar es salaam,Mwalimu Faustine Byalile akiwakabidhi keki wanafunzi wa Shule ya Msingi King'ong'o iliyopo Kata ya Saranga wilaya ya Ubungo mkoa wa Dar es salaam kwenye kwenye maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyo fanyika katika viwanja wa shule hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...