Na Amiri Kilagalila,Njombe


Sekretarieti ya Chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Njombe imewatahadharisha wanachama wa Chama hicho pamoja na viongozi kwa kushindwa kulipa kadi zao za uanachama kwa wakati huku wengine wakisubiri nyakati za uchaguzi na kuanza kulipia.

Katibu wa Chama cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Njombe Bi,Amina Imbo amesema wanachama wengi hususani wanaohitaji kugombea nafasi za uongozi ndani ya Chama hicho wamekuwa wakijitokeza kulipia kadi zao hususani katika wakati huo ili chama kiwape nafasi za kugombea nafasi.

Ameyasema hayo wilayani Makete mkoani Njombe wakati akitoa semina ya uimarishaji wa uchumi wa Chama na jumuiya zake katika ziara ya Sekretarieti ya Chama mkoa inayozunguka halmashauri 6 za mkoa huo kwa ajili ya kukagua uhai wa Chama na jumuiya zake,kukagua utekelezaji wa Ilani (miradi mbali mbali ya Maendeleo) pamoja na utekekelezaji wa maagizo mbali mbali kutoka ngazi ya juu ya Chama.

Bi Amina amepiga marufuku utaratibu huo na kuagiza kila mwanachama kulipia kadi yake ya shilingi 100 kwa mwezi na kwa wakati ili kuendelea kuimarisha uhai wa Chama kwa kuwa pia uhai wa mwanachama hutegemea na ulipiaji wa kadi kwa wakati kwa kuwa chama hicho kimekuwa na wanachama wengi wasio hai.

"Tutaenda kwenye kompyuta na kuangalia uhai wako kwa kulipa ada yako ya kila mwezi bila limbikizo iwe kwa mwezi,miezi mitatu,mitano au hata mwaka na ndio itakuwa sababu ya anayetaka kugombea uongozi kumpa kipaumbele katika nafasi"alisema Amina Imbo

Aidha ameagiza viongozi wote wa CCM kuweka mikakati mizuri ya uingizaji wa wanachama wapya kwa kuwa chama hicho mkoa wa Njombe kina wanachama Laki moja na stini pekee wakati taifa limeelekeza angalau mkoa kuwa na wanachama zaidi ya laki tano hatua  inayopelekea mkoa wa Njombe kuwa katika nafasi mbaya kwenye takwimu za idadi ya wanachama.

Katibu wa UWT mkoa wa Njombe Bi,Frola Kapalie ametoa rai kwa wanachama kuongeza nguvu katika ulipiaji ada ya uanachama kwa kuwa mfumo wa sasa umekuwa ukionyesha taarifa za kila mwanachama.

“Tujitafakari na kuhakikisha tumelipia kadi kwa kuwa viongozi wanatazama kwa karibu mwenendo wa uanachama wetu"alisema Frola

Kwa upande wake Katibu wa siasa na uenezi mkoa wa Njombe Erasto Ngole ameagiza viongozi kuandaa na kufanya vikao vya uongozi kila wakati ili kujiimarisha na kupeleka ajenda za vikao na maendeleo ya Chama kwa wanachama

"Mkikaa na kukubaliana baadhi ya ajenda kwa utaratibu na makatibu kata wakaandika vizuri taarifa za vikao tunaamini vikao hivyo vitakuwa halali na sio vya majungu na Chama kitakuwa vizuri na kwa utaratibu"alisema Ngole

Wilbath Mwalyoyo na Matrida Msigwa ni baadhi ya wanachama na viongozi wa CCM katika ngazi za kata wilayani humo walioshiriki katika semina hiyo,wameshukuru kutembelewa na viongozi hao na kukumbushwa namna ulipaji wa ada pamoja na uingizwaji wa wanachama wapya ndani ya Chama hicho.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...