NA  YEREMIAS  NGERANGERA…NAMTUMBO

Akitoa taarifa  kwenye kikao  cha kamati ya lishe ya wilaya ya Namtumbo  mratibu wa kamati ya lishe Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo  bwana  Sosteneth  Mumba  alisema  kuwa kwa kipindi cha mwaka mmoja  2020/2021 Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo  imewabaini watoto 35 wenye utapiamlo mkali

Mumba  alidai watoto  35 kuanzia miezi sita  na chini  ya miaka mitano  waliobainika walitokana na kuwapima watoto  10,689 katika kata 21 na vijiji 66.ambao  kati ya hao 35 ndio waligundulika na utapiamlo mkali katika Halmashauri ya wilaya Namtumbo.

Mtendaji wa kata ya  Rwinga  bwana Mario  Mwageni  alilalamikia ugumu  wa ukusanyaji taarifa za lishe katika kata yake  akidai kata yake haina watendaji wa  vijiji  kutokana na kata hiyo kuwa sehemu ya mamlaka ya mji mdogo wa Namtumbo  hivyo kuwatumia wahudumu  ambao  sio waajiriwa wa serikali  wanafanya kazi hizo za kukusanya  taarifa za lishe  watakavyo  wao  .

Aidha  bwana  Mwageni aliongeza  kuwa  wahudumu ngazi za vijiji wanapaswa  kutoa  elimu  kupitia mikutano ya hadhara ya vijjji  kwa kushirikiana na watendaji wa vijiji ili kuelimisha jamii iweze  kuelemika katika swala la lishe  na kuepukana na utapiamlo.

Mwenyekiti wa kamati ya lishe wilaya ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Namtumbo Julius  Kenneth Ningu aliwataka watendaji wa kata,vijiji kwa kushirikiana na wahudumu wa afya ngazi za vijiji kutoa taarifa zenye  uhalisia kuhusu hali  ya lishe katika mazingira yao .

Ningu pamoja na mambo mengine aliwataka pia watendaji kupitia mikutano ya vijiji kutumia muda wao kutoa elimu ya lishe kwenye vikao vyao kwa kuwaalika wataalamu ili kuwaelimisha wananchi kuzingatia maswala ya lishe kikamilifu ili kupunguza watoto wapatao utapiamlo  katika wilaya ya Namtumbo .

Kikao cha kamati ya lishe wilaya  kimefanyika  kwa lengo la kutoa taarifa ya hali ya lishe katika wilaya ya Namtumbo ambapo kwa kipindi cha mwaka mmoja 2020/2021 watoto 35 kati ya 10,689 wamegundulika kuwa na utapiamlo  mkali wilayani Namtumbo.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...