·         Watu kujifunza namna ya kujiendeleza kielimu na kuendesha biashara mtandaoni

Zanzibar. Jumatatu, Julai 19, 2021. Kampuni ya simu ya ZANTEL leo imezindua kijiji cha kidigitali, eneo ambalo limewekwa miundombinu imara ya intaneti kwa lengo la kutoa mafunzo kwa wakazi wa Zanzibar namna bora ya kutumia mitandao katika kujiendeleza kielimu na kibiashara.

Hatua hii ni miongoni mwa utekelezaji wa kampeni ya ‘Pasua Anga Ki Zantel 4G’ awamu ya pili, ambayo pamoja na mambo mengine ina lenga kutoa elimu kwa wakazi wa Zanzibar juu ya umuhimu wa mtandao wa 4G katika kuleta maendeleo ya kijamii na uchumi.

Mpango huo ni sehemu ya mkakati wa Zantel wa kuchochea mageuzi ya kimtandao na kufanya watu waishi kidigitali.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Meneja Masoko wa Zantel-Zanzibar, Rukia Mtingwa alisema kuwa kituo hicho cha Kiditali kitatoa huduma za kimtandao bure kwa wakazi wa Zanzibar ndani ya miezi miwili.

Sehemu hii ina wataalamu na wabobezi wa huduma hizo za Elimu na Biashara za mtandaoni ambao watakuwa wakitoa mafunzo kwa watu watakaofika hapa, namna ya kutumia mtandao wa 4G kupata huduma hizo,” alisema.

“Elimu ya mtandaoni si kwa ajili ya wanafunzi wa shule na vyuo tu, bali hata kwa watu wenye vipaji mbalimbali na wafanya biashara wanaweza kujifunza kupitia mtandao namna bora ya kukuza na kutangaza kazi zao na kuboresha. Kwa mfano leo hii tuko na Said Sugu ambaye yeye ameweza kutengeneza magari, helikopta kwa kutumia kipaji chake na mtandao kuongeza ujuzi,” alisema

Wafanya biashara pia wana fursa ya kupata masoko mapya mtandaoni. Wakiwa hapa katika kijiji cha kidigitali, watafundishwa namna rahisi ya kutumia mitandao kuuza na kutangaza biashara zao.

Pamoja na hilo, Zantel imezindua shindano la kidigitali ambalo linatoa fursa kwa watu mbalimbali kuonesha vitu ambavyo wamejifunza na kutengeneza kwa kutumia mtandao na kujishindia zawadi hadi Sh300,000.

“Unachotakiwa kufanya ni kutengeneza video fupi na kuipost kwenye mtandao wa kijamii na kutag kurasa za Zantel.Video ambayo itapendwa zaidi itajishindia zawadi hadi Shilingi 300,000,” alisema.

 

Meneja Masoko wa Zantel-Zanzibar,Rukia Mtingwa akifurahia jambo na mgunduzi wa teknolojia, Said Sugu wakati wa uzinduzi wa Kijiji cha kidigitali ‘Digital Village’ ambacho ni maalumu kwaajili ya watu kujifunza matumizi ya mtandao wa 4G. Kulia ni Soud Hassan, mbunifu wa teknolojia.Wagundunduzi hao wamefanikisha kutengeneza vitu mbalimbali ikiwamo helikopta na magari wakitumia kipaji na intaneti kama nyenzo ya kujifunzia.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...