Aliyekuwa mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) wilaya ya kahama kwa mwaka 2017/19, Samson Lutema Lutonja amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuchaguliwa na chama cha mapinduzi (CCM) kugombea ubunge wa jimbo la ushetu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo  muda mfupi baada ya kuchukua fomu katika ofisi za chama cha mapinduzi wilayani hapa Lutonja amesema amedhamiria  kuwaunganisha wananchi wa jimbo ushetu  katika sekta ya  elimu, afya, maji na miundombinu ya barabara.

“Nitaanzia pale alipoishia mtangulizi wetu aliyetangulia mbele za haki kama chama changu kikiniparidhaa ya kugombea jimbo la ushetu,Elias Kwandikwa alifanya mambo mengi katika jimbo hili,nitayaishi mazuri yake,”alisema Lutonja.

Amesema kuwa kupitia uzoefu alioupata ndani ya chama wakati akiongoza umoja wa vijana wilaya ya kahama (UVCCM) utamsaidia kuongoza kwa weledi pindi atakapopata nafasi hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...